Tuesday, 5 November 2013

YOHANA MORRIS
         STOPPER WA MBEYA CITY.

      Yohana morris  ni mmoja kati ya wachezaji waliofanikisha kuipandisha Mbeya City,ni beki kisiki ambae ana uwezo wa kucheza namba nyingi bila shida yeyote.ana uwezo wa kucheza beki wa kulia pembeni au hata kushoto,na pia anacheza bila shida nafasi zote za kati za ulinzi.

                Yohana amezaliwa katika familia ya soka kwani kaka zake wote walikua ni wachezaji,  kuanzia kaka mkubwa ambae ni afisa wa magereza mororgoro alikua ni mchezaji mahiri wa timu ya magereza,  kaka yake mwingine Osward Morris nae amecheza sana katika ligi kuu ya Tanzania akiwa na timu ya Prisons na sasa hivi ni kocha msaidizi wa timu hiyo,  wakati  mwingine ni Henri Morris ambae alicheza kwa mafanikio katika timu zaPrisons Yanga,Miembeni  ya Zanzibar, na baadae Moro United.
      Yohana  alizaliwa mkoani Morogoro na kupata elimu yake ya msingi hapo hapo Morogoro,na toka akiwa shule ya msingi alionyesha uwezo mkubwa sana wa soka na kumfanya muda mwingi autumie kucheza mpira.
    Baadae alihamia  Mbeya kwa kaka yake Oswardn huko ndipo kocha  maarufu Josef Kanakamfumu akamuona na kuvutiwa na kipaji chake,  akaongea na waalimu wa shule ya Makongo akapelekwa kusoma sekondari pale
Alipomaliza form four akajiunga na academy moja iliyokua ikiitwa KICK OFF, na huko akashiriki mashindano kadhaa yakiwemo maarufu ya ROLLING STONE.

          Wakati timu ya Mbeya City inaanzishwa,  kocha Juma Mwambusi  akamwita  na kua ni mmoja wa waanzilishi wa timu hiyo,  wakaanza toka daraja la tatu lakini bahati nzuri uongozi ukainunua timu ya RHINO iliyokua daraja la kwanza,hivyo automatic wakacheza ligi daraja la kwanza lakini bahati mbaya hawakufanikiwa kupanda daraja,na ndipo msimu uliofata  wakajitayarisha vizuri na kufanikiwa kupanda hadi ligi kuu ya Tanzania. Ameweza kucheza mechi kadhaa na hajawaangusha wapenzi wa Mbeya City,  kwani katika mechi waliyocheza na Yanga jijini Mbeya alikua ni sumu kwa washambuliaji  hatari wa timu hiyo,Kavumbagu na Jerry Tegete,na hata katika mchezo waliocheza na Simba alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwabana washambuliaji wa timu hiyo.

     Ukiondoa makosa kidogo yaliyofanywa mwanzoni mwa kipindi cha kwanza na kusababisha magoli  mawili ya haraka toka kwa Amis Tambwe, aliweza kumshika mshambulaji hatari wa SIMBA Betram Mombeki na hivyo kuzuia mashambulizi na hatari zote zilizotakiwa kuja katika goli lao….
  


     

No comments:

Post a Comment