Saturday, 14 December 2013

Arsenal yachezea

Arsenal imepoteza mchezo wa pili mfululizo baada ya kufungwa na Man City kwa magoli 6-3 katika mchezo ambao kiungo wa Man City Fernandinho alichaguliwa kua ni mchezaji bora wa mchezo huo.
        Ingawa Arsenal ndio walikua wa kwanza kulishambulia goli la City baada ya Jack Wilshere kupiga shuti lililotoka nje ya goli katika dakika ya 11, lakini Man City ndio walikua wa kwanza kupata goli  baada ya kona iliyopigwa  na David Silva kugongwa kidogo na kichwa na Martin Demichelis na kumkuta Sergio Aguero aliyepiga na kutinga golini.

      City waliendelea kulisakama lango la Arsenal na Negredo nusura aifungie timu yake baada ya kupewa pasi nzuri na Kompany lakini akapiga shuti lililotoka nje ya uwanja.

   Arsenal walisawazisha baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Aaron Ramsey baada ya kumnyang’anya mpira Yaya toure na kutoa pasi nzuri  kwa Mesut Ozil aliyeingiza mpira ndani na kumkuta Theo Walcot aliyepiga shuti na kuandika bao.

     City waliongeza bao la pili baada ya pasi kutoka kwa Yaya Toure kumkuta Pablo Zabaleta aliyepiga krosi fupi na Negredo akakutana nayo na kuifungia City bao la pili.

             Wakati wa kujaribu kuokoa hilo goli beki wa Arsenal Koscielny aliumia na kutolewa.

            Goli la tatu la City lilipatikana baada ya Matheu Flamini kushindwa kuzuia pasi aliyopigiwa na Sagna na Fernandinho akauvuta na kupiga shuti la kiufundi lililomshinda kipa wa Arsenal.

        Arsenal hawakukata tamaa  na Walcot aliongeza bao la pili baada ya kazi nzuri iliyofanywa tena na Aaron Ramsey.

       Walikua ni City  walioongeza bao baada ya Jesus Navas kupiga krosi nzuri na  Silva alimzidi kasi beki wa Arsena Mertesacker na kuupiga  mpira na kufunga.

       Fernandinho akaongeza bao la 5 baada ya kuupiga mpira uliomshinda kipa wa Arsenal.

      Mertesacker aliongeza goli kwa Arsenal baada ya kupiga kichwa cha kiufundi na baadae Yaya Toure akafunga goli la 6 kwa City kwa njia ya penati baada ya kipa wa Arsenal kumfanyia faulo Fernandinho aliyekua akitaka kufunga.
    

         

No comments:

Post a Comment