Saturday, 14 December 2013

Kwa mwalalika

Mashine ya Mwalalika ipo karibu na shule ya msingi Itiji, ni sehemu maarufu sana kwa wakazi wa Mbeya,ilianzishwa miaka ya sitini na mzee Haji Mwalalika,na baadae alipokuja kufariki kwa ajali ya tractor akiwa pamoja na mwanawe Sadiki mwanzoni mwa miaka ya 80 ikaendelezwa na mwanae mwingine aliyeitwa Athumani.

           Ni mashine iliyokua ikihudumia watu wengi sana kusaga nafaka zao, watu kutoka Majengo,Ghana na hata Soko Matola walikua wakitegemea mashine hii kusaga vyakula vyao. Kina mama wengi waliokuwa wakifanya biashara ya pombe za kiennyeji katika kilabu maarufu cha lejiko nao walikuwa wakijaa sana katika mashine hii ili kununua pumba za kutayarishia pombe.

        kabla ya kuanzishwa kwa mashine hii kulikua na mashine nyingine iliyokua chini kidogo kuelekea mabatini,ilikua ni ya mtanzania mwenye asili ya kiasia alijulikana  kwa jina la Punja(sijui alitokea sehemu za Punjab India?), ingawa alikua na jina lake lakini watu wa wakati huo waliamini kipimo chake kilikua kinapunja na kubakisha unga katika mashine!!!!!ingawa si ukweli bali ni tetesi zilizozoeleka hadi ikawa kama ukweli,ndipo akapata hilo jina la Punja.nae alidumu na baadae akawauzia waswahili na ilikuwepo hadi miaka ya tisini mwishoni.

      Kwa wakazi wa Mbeya watakua  wanakumbuka mashine zilizokuwepo miaka ya themanini hadi tisini,zilikua ni za kuhesabika,ilikua ya Mwalalika,ya Punja na juu kabisa majengo ilikuwepo ya Bahati,kwa wakati ule zilikua zinafanya sana kazi kwani viwanda vya kusaga nafaka vilikua bado havijaanza kufanya kazi sehemu kubwa ya Tanzania.

 

No comments:

Post a Comment