Saturday, 7 December 2013

CHELSEA HOI….

Hull City imepata ushindi mnono nyumbani baada ya kuwafunga Chelsea kwa magoli 3-2 katika mchezo mzuri uliojaa ufundi pande zote.
      Chelsea walikua wa kwanza kupata bao lililofungwa na Schuerrle aliyepokea pasi toka kwa Obi Mikel na kumpiga chenga mara mbili beki wa Stoke City Shawcross  kisha kupiga shuti la kiufundi lililomshinda kipa Begovic.

    Stoke walipata bao la kwanza baada ya kosa lilofanywa na kipa wa Chelsea la kutaka kutoka na kuamua kurudi hivyo kuwachanganya mabeki na ndipo Peter Crowch akautuliza mpira na kufunga kirahisi.

       Stoke waliongeza bao baada ya Jonathan Walter kumpita Cezar Azpilicueta  na kutoa pasi kwa Steven Ireland aliyepiga shuti lililokatika na kutinga wavuni.

     Lakini Chelsea wakasawazisha kwa  goli lililofungwa tena na Schuerrle baada ya faulo iliyopigwa na Mata kuokolewa na mpira kumkuta mfungaji aliyepiga shuti na kuingia golini.

     Stoke walipata goli la ushindi kupitia kwa Oussama Asaidi aliyepokea pasi toka kwa Ireland na kukimbia na mpira kisha kupiga shuti lililomshinda kipa wa Chelsea na kuandika goli la tatu.

     Hadi mchezo unakwisha Stoke 3 na Chelsea 2.

     


No comments:

Post a Comment