Tuesday, 10 December 2013

Juma ahmad
Kipa wa mecco na tukuyu stars

        Alizaliwa Mbeya Soko Matola na kusoma shule ya msingi Mbata mahali ambapo ndipo alianza kucheza soka kama golikipa, akiwa na watoto wengine  wa uswahilini kama kina Allen Simumba,Mbaraka Kaparata,Amani Masebo na wengine wengi wa soko Matola na maeneo ya Ghana.
         
Wakati akiwa darasa la saba yeye pamoja wenzake walichukuliwa na mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Said Mkwanda  ambae alikua na timu iliyokua maarufu sana jijini Mbeya ya Town Stars huko walikutana na vijana wengine ambao tayari walikua wametangulia kama kina Peter Poka, Juma  Songoro “TOZZO” na wengine ambao walikua ni wakubwa kwao kama kina Haji Abas,Kakoko na kina King Kubenda na mchanganyiko wao ulikua ni timu moja iliyokua kali na inatisha sana jijini Mbeya.
Kutok kushoto waliosimama-Saleh Abdulrahman,Samuel Kakoko,Yona,John,Justin Mwasa,Franklin Mwafwenga,Allen Simumba,Joel Simumba,Omar Masanja,,Saidi,Juma Songoro (tozzo),John,Said Mkwanda (faza)na Juma Ahmad.
waliochuchumaa ni Abdallah Mwasimba,Amani Masebo,Mbaraka Kaparata,King kubenda,MaisaraMwakibinga, Matola(friend)na Mussa Mwaiposa.
     Alipofika Town Stars haikuchukua muda pamoja na udogo wake lakini aliweza kupata namba, hivyo alicheza   huku akishirikiana na Peter Poka na hata baadae Poka alipoondoka akabaki kua ni kipa namba moja.
       Baadae akachukuliwa na timu ya Mecco, na alishiriki katika kuipandisha daraja toka daraja la pili hadi daraja la kwanza (sasa ni ligi kuu ya Vodacom)
TIMU YA MECCO,kutoka kushoto waliosimama Ayoub,Ephraim Kayeta,Betwel Africa,Mario Mkongwa,Juma Ahmad,Gama,na Laiton Mbogi. Waliochuchumaa ni John Moses Kaniki,Seif Shwari,Mbaga Mwintika,Nasibu Abas,na Nurdin Kasabalala.
      Mecco alikutana na wachezaji wengi na kutoka sehemu tofauti za Tanzania, kama kina  Moses  Kaniki,Mbaga Mwintiku, Nasib Abas,George Mangula, Danny Magogo,Nurdin na Abeid Kasabalala na wengine wengi.
        Akatoka MECCO na kuchukuliwa na Tukuyu Stars  iliyokua pia katika ligi kuu na akacheza kwa mafanikio kwa misimu mitatu.
Juma Ahmad akidaka mpira,nyuma yake Salum Kussi,na Godwin Aswile,mbele Abeid Mziba na Mohamed Kassanda,  wakati TUKUYU STARS ilipocheza na YANGA.
         NaTukuyu Stars alikutana na wachezaji wengi wenye vipaji vikubwa sana kama vile kina Mohamed Kasanda,Justin Mtekere,Emanuel Mwambipile,Ikupilika Nkoba na Peter Luis ambao waliifanya timu ya Tukuyu kua ni moja kati ya timu bora sana zilizowahi kutokea nchini Tanzania.
TUKUYU STARS kutoka kushoto Mohamed Kassanda,Suleiman Mrisho,Assanga Aswile,Issah Mohamed,,Pio Mwashitete,Jabir Mohamed (jeby),na Gamshad Gaudast.WALIOCHUCHUMAA Kanza Mrisho,Raphael Mapunda,Ikupilika Nkoba,Juma Ahmad,Chchala Muya,Robson,Daudi Kufakunoga,na Michael Kidilu.
            Akiwa Tukuyu Stars aliweza kucheza mechi karibu zote za ligi na kati ya hizo ni pamoja na michezo migumu waliyocheza na timu za Simba na Yanga.
Juma Ahmad  akiudaka mpira huku Mohamed Kassanda akimzuia  Edward Chumila
        Baadae akahamia Tiger ya Tunduma alikokaa msimu mmoja na kisha kwenda  Reli ya Morogoro alikokaa hadi anastaafu kucheza soka.

        Kwa sasa Juma Ahmad anafanya kazi Gymkhana Dar na pia ni golikipa wa timu hiyo ya Gymkhana.
       
      





No comments:

Post a Comment