Thursday, 12 December 2013

Stars yakosa nafasi ya tatu

Kilimanjaro Stars imeshindwa kupata nafasi ya tatu baada ya kufungwa kwa penati 6-5 na Zambia katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa mashindano ya CECAFA senior challenge cup.

       Hadi muda wa kawaida unamalizika timu hizo zilikua sare kwa goli moja kwa moja  kwa magoli yaliyofungwa na Ronald Kampamba wa Zambia aliyefunga baada ya kumtoka beki wa Stars Said Morad na kupiga shuti la chini lililompita kipa wa Stars Ivo Mapunda.
       Mbwana Samata aliisawazishia Stars kwa goli zuri la kiufundi baada ya kumzunguka beki wa Zambia na kupiga shuti kali la kushtukiza la mguu wa kushoto na kumshinda kipa wa Chipolopolo.
             Felix Katongo na Ronald Kampamba walifunga penati mbili za kwanza kabla ya Mbwana Samatta na Erasto Nyoni nao kufunga mbili za Stars, kisha Justin Zulu akakosa baada ya kugonga mwamba, na kwa Stars Himid Mao akafunga.
       Captain wa Zambia Bronson Chama akaifungia Zambia penati ya nne kabla ya Amri Kiemba nae hajafunga ya nne na kuifanya Stars iwe mbele kwa penati 4-3. Julius Situmbeko akaifungia Zambia penat ya mwisho na ikabaki moja kwa Tanzania lakini Athman Chanongo akapiga penati iliyookolewa na kipa wa Chipolopolo Titima.
       Baadae zilipoongezwa moja moja Ramadhani Singano na Rodrick Kabwe wakapata penati zao kabla ya Ivo Mapunda kuokoa penati iliyopigwa na Konwan Mtonga. Ikabaki kwa Mrisho Ngasa kumalizia lakini nae penati yake ikaokolewa na kipa wa Zambia.
    Kabaso Chongo akaipatia timu yake penati iliyofuata kisha Kelvin Yondani akapiga penati liyookolewa na kipa wa Zambia na kuwafanya Zambia kushika nafasi ya tatu kwa penati 6-5.

        

No comments:

Post a Comment