Monday, 16 December 2013

MAN UNITED YASHINDA

Magoli mawili ya haraka haraka yaliyofungwa na Dany Welbeck  na jingine lililofungwa na Tom Cleverley yalitosha kuwafanya Man united kupata ushindi katika ligi ya Uingereza baada ya kupoteza michezo miwili mfululizo.

      Antonio Valencia alikua katika kiwango kizuri na kuisumbua san na ngome ya Aston Villa, kwani alikua akishirikiana vizuri na Rafael hivyo kuwapa kazi ngumu mabeki wa Villa.

      Man walipata bao la kwanza dakika ya 15 kupitia kwa Welbeck aliyekutana na mpira uliogonga mwamba baada ya  Rafael kukimbia na mpira na kupiga krosi ya nguvu  iliyomkuta Januzaj aliyepiga kichwa na mpira ukagonga mwamba.
      Welbeck aliwahi kuufikia kabla ya mabeki hawajajipanga na na kufunga goli lake la kwanza katika ligi msimu huu.

        Kabla ya Villa hawajatulia, beki wao Nathan Barker alipoteza mpira na ukachukuliwa na Welbeck aliyempelekea Valencia ambae nae akapiga krosi ya chini chini na mpira kumkuta Welbeck aliyefunga goli la pili. Hiyo ilikua ni dakika ya 18.

    Man waliutawala mchezo na Valencia akawa tishio zaidi alitoa pasi nyingi za kusababisha magoli lakini zilipotezwa na washambuliaji wa Man.
     Kipa wa Man alikua muda mwingi wa mchezo hana la kufanya kwani washambuliaji wa Villa hawakua kabisa na madhara na hata mchezaji wao hatari Christian Benteke alikua hana msaada mkubwa,  hadi sasa amecheza michezo kumi bila ya kufunga goli.

   Man walipata bao la tatu katika dakika ya 52  kupitia kwa Cleverley  aliyepigiwa pasi nzuri a Wayne Rooney.

       Darren Fletcher aliingia katika dakika ya 70 baada ya kutokuwepo uwanjani kwa kipindi kirefu kutokana na maradhi.

      

         Fletcher aliichezea Man mara ya mwisho tarehe 26 december mwaka jana, hivyo alipokelewa kwa furaha na mashabiki wa timu hiyo. 

No comments:

Post a Comment