MOURINHO; CHELSEA HAINA WAFUNGAJI
Pamoja kua na washambuliaji mahiri kama
Fernando Torres, Samuel Etoo, na Demba Ba, lakini kocha wa Chelsea Mourinho
amesema timu yake haina washambuliaji wa kuweza kuwapatia ubingwa.
Chelsea walifungwa na Sunderland kwa
magoli mawili kwa moja katika mchezo wa kombe la ligi(Capital one).
Chelsea walipata bao lao katika dakika ya
kwanza ya kipindi cha pili baada ya Beki wake wa kulia Azpillicueta kukimbia na
mpira na kupiga krosi ya chini chini iliyomkuta Lampad akiwa na beki wa Sunderland Lee Cattermole na wakaugonga mpira lakini
ukoakolewa na kipa ukiwa umepita kidogo mstari wa goli.goli hilo alikuja kupewa Cattermole.
Chelsea baada ya kupata hilo bao
waliendelea kushambulia na baadae beki wa Sunderland Craig Gardner alikosea na
kupiga pasi iliyomkuta Etoo lakini akashindwa kufunga baada ya kuupiga mpira
nje.
Sunderland walisawazisha zikiwa
zimebaki dakika mbili mpira kumalizika baada ya mpira aliopiga Altidore kuokolewa vibaya na kumkuta Borini aliyepiga
shuti lililomshinda kipa wa Chelsea.
Katikati ya mchezo huo mtu mmoja ambae alikua amevua shati lake aliinia kati kati ya uwanja na kuufanya mchezo huo kusimama kwa muda.
Sunderland waliongeza bao la
pili zikiwa zimesalia tena dakika mbili za nyongeza wakati Borini alipotoa pasi
nzuri kwa Ki aliyejitengenezea nafasi na kupiga shuti lililoingia golini na
kuwafanya Chelsea watolewe katika kombe la ligi.
Akiongea
baada ya mchezo huo kocha wa Chelsea Jose Mourinho alisema tmu yake imekosa
washambuliaji wenye uchu ndio maana hawapati magoli.
Katika magoli 32
yaliyofungwa na timu hiyo katika ligi ni magoli matano tu yaliyofungwa na washambuliaji.
Demba ba kafuga moja, Samuel Etoo kafunga mawili na Fernando Torres nae kafunga
mawili.








No comments:
Post a Comment