Wednesday, 18 December 2013

Stoke hoi kwa man utd

MAN united imefanikiwa kuingia katika nusu fainali ya kombe la ligi(capital one)baada ya kupata ushndi wa goli 2-0 dhidi ya timu ngumu ya Stoke City.

       Katika mchezo huo uliochezwa huku kukiwa na hali mbaya ya hewa kutokana na mvua na upepo mkali uliokua ukiambatana na barafu,man walipata mabao yake yote mawili katika kipindi cha pili cha mchezo huo.

        Mchezo ulisimamishwa dakika ya 29 baada ya hali ya hewa kuzidi kua mbaya na mwamuzi wa pambano kuamua kuusimamisha mpira hadi hali itakapotulia.mchezo ulisimama kwa dakika kumi.

        Goli la kwanza lilifungwa na Ashley Young katika dakika ya 62 baada ya faulo iliyopigwa haraka haraka na Cleverley na Young akampasia Chicharito aliyemrudishia Young na akapiga shuti kali sana lililomshinda kipa wa Stoke.

      Young alishngilia sana goli hilo kiasi akaaumua kwenda kushangilia na mashabiki, hali iliyosababisha muamuzi kumpa kadi ya njano.

        Stoke nao hawakukata tamaa kwani walishambulia goli la Man wakiongozwa na kiungo wao makini Steven Ireland, lakini beki ya Man ikiongozwa na Chriss Smalling na John Evans walikua wakifanya kazi nzuri ya kuzuia mashambulizi hayo.

         Jonathan Walters wa Stoke alifanikiwa kuwapita mabeki wa Man lakini shuti lake lilikamatwa na kipa David De Gea.

        Man walipata bao la pili kupitia kwa beki wao Patrice Evra aliyeingia katia 18 ya Stoke na kupiga mpira mzuri kwa kutumia mguu wa kuli na kuweza kuandika goli la pili.


      Kwa matokeo hayo Man United watakutana na timu ya Sunderland katka nsu fainali ya mashndano hayo.

No comments:

Post a Comment