Friday, 24 January 2014

KI MJINI MJINI
MBEYA MJINI (picha kwa hisani ya Haneef Lohaar)

Ogopa sana kuibiwa au kutapeliwa unapokua mjini, wengi wanaoibiwa au kutapeliwa ni wale wanaojiona ni wajanja sana na wa mjini sana kiasi wanajiamini kupita kiasi, wanasahau kwamba hao wezi na matapeli nao maisha yao ni ya mjini kila siku na wanaishi kwa kazi hiyo hivyo kila mara wanabadili mbinu na mitindo ya kufanyia kazi, ni sawa na mfanyakazi yeyote anaeenda kuongeza elimu chuoni,nao pia wana elimu ya mtaani wanayoongeza kila mara wanaiita “STREET WISE”……na degree yake ni ngumu kupata lakini ukiipata unakua kweli umefaulu…..

         Ninajaribu kuandika mbinu mbali mbali zinazotumika na wezi au hao matapeli katika kufanikisha kazi zao, ingawa hizo mbinu zinabadilika mara kwa mara.
1-UKIENDA  mjini, muangalie sana anaekuelekeza upaki gari yako vizuri….. mara nyingi anakuelekeza kisha unapofunga mlango kwa funguo yeye anakua kaushika mlango mmoja kitasa kinakua juu hivyo uki lock huo mlango unabaki wazi, UNAPOONDOKA ANAUFUNGUA NA KUKUIBIA……. Hivyo hakikisha unaitazama milango yote kama imefunga ndio uondoke.
2.-UKIWA na laptop au kitu cha thamani weka katika buti la gari, usiweke mbele au kwa urahisi zaidi mwambie fundi akutengenezee sehemu ya kuweka laptop chini ya kiti cha dereva-maana mara nyingi hua wanachungulia kama kuna laptop au begi lolote na linawapa hamu ya kuvunja drisha na kuiba
3-USIONE ushamba kuweka alarm hata mbili katika gari lako kwani ni rahisi sana kufungua milango au kuvunjiwa kioo kidogo cha nyuma ya gari na kuibiwa kila kilichomo  zikiwemo power window……
      (kuna njia nyngi wanazotumia kuvunja vioo au kufungua milango. Wanaweza kuweka jiwe katika kigunia na kuvunja husikii kelele, wanaweza kuchukua ile risasi nyeusi ya ndani ya plug za gari, wanasaga na kuchanganya na maji wakimwagia katka kioo kinaachia taratibu, au kufungua mlango hua wanachukua mpira mdogo wa tenis (kitenes)wanaukata katkati, kisha wanauweka katika tundu la funguo mlango wa mbele, linajaa kabisa hewa kisha wanapiga kwa nguvu lock inafunguka)HIVYO SULUHISHO NI KUWEKA ALARM MBILI MAANA HAIWEZEKANI KUZIPIGA SHOTI ZOTE MBILI..
4-UKIBEBA laptop barabarani hakikisha unaiweka upande ambao sio wa barabarani, kwani mara nyngi wanakuja kwa nyuma na gari au piki piki na kukuvuta beg na kukimbia nalo hivyo ukiweka upande wa pili inakua ngumu……
5- KWA WALE  wanaotafuta nyumba au vyumba vya kupanga mjini, hakikisha dalali akikuonyesha nyumba na mwenye nyumba, nenda kwa jirani yeyote hapo karibu ndio uulize tena usikubali mara moja, maana wengi hua ni wajanja na wezi, kwa uhakika ukionyeshwa nyumba ondoka baadae rudi hata katika duka la jirani ndio uulize tena muhusika ni nani ili ujiridhishe.

6-NA KWA WALE WENZANGU  wanaopenda kununua dawa za kuongeza nguvu za kiume za kienyeji kwa wamasai au kwa yeyote mara nyingi ni za utapeli, kwani wanalofanya hao wamasai  ni kwenda duka la dawa kisha wananunua vidonge vya kuongeza nguvu(kama electro au Viagra)kwa buku 3 dozi kisha anaisaga na kuchanganya na unga anaojua yeye kua sio sumu kisha anakuuzia kuanzia buku kumi…..na ukijaribu unaona booonge la mganga  NA KUJIONA UNA NGUVU BALAA kumbe umepigwa changa la macho…………

No comments:

Post a Comment