RHINO HOI KWA SIMBA
TIMU
YA Rhino ya Tabora imeshindwa kutamba
mbele ya Simba baada ya kufungwa kwa goli moja kwa bila katika mchezo ligi kuu ya Vodacom Tanzania uliochezwa katika uwanja wa taifa Dar es salaam.
![]() |
| WACHEZAJI WA SIMBA WAKISHANGILIA GOLI LA SINGANO HUKU RHINO WAKILAUMIANA |
Goli la Simba lilipatikana mwanzoni mwa
kipindi cha kwanza kupitia kwa nyota wa timu hiyo Ramadhani Singano aliyepiga
shuti kali baada ya kukutana na mpira uliiokolewa vibaya na mabeki wa Rhino
kutokana na kiki ya Ally Badru.
![]() |
| ALLY BADRU AKIPIGA SHUTI |
Kwa ujumla muda mwingi mchezo ulikua wa
taratibu ingawa ni Simba ambao walipanga mashambulizi mengi langoni mwa Rhino, lakini hawakuweza kumpita kirahisi kipa wa
timu hiyo aliyeokoa hatari kadhaa ikiwemo penati iliyopigwa na Ramadhani
Singano
![]() |
| SIMBA WAKISHANGILIA |
Penati hiyo ilitokana na beki wa Rhino
kuushika mpira uliokua ukielekea golini kufuatia shuti lililopigwa na Haruna
Chanongo.
Amisi Tambwe aliweza kufanikiwa
kufunga mara mbili lakini mwamuzi mara zote akikataa , mara ya kwanza
aliunganisha krosi iliyopigwa na Singano lakini wakati mwamuzi akiashiria kua
ni goli, msaidizi wake alilikataa, na mara ya pili aliusindikiza mpira
uliomshinda kipa lakini pia mwamuzi akasema kuna madhambi yalifanyika.
![]() |
| SINGANO AKIMTOKA BEKI WA RHINO |
Pamoja na Singano kufunga hilo goli moja, lakini alipoteza nafasi nyingi sana za kufunga kutokana na uhodari wa kipa au kutokua makini.
Kocha wa Simba Loga alimuingiza Betram Mombeki
na baada ya kucheza kwa dakika sita akaamua kumtoa kwa sababu alikua amekosea
mara tatu na nafasi yake ikachukuliwa na Henry Joseph, jambo lililozua malalamiko
toka kwa mashabiki kwamba kocha hajamtendea haki Mombeki.





No comments:
Post a Comment