Thursday, 20 February 2014

Anthony matogoro 
Mpiganaji wa mbeya city

 
     Mmoja kati ya wachezaji wanaotamba katika timu ya Mbeya City  ni Anthony Matogoro, Kiungo wa chini  anaekaba toka mwanzo wa mchezo hadi mwisho, ni mpiganaji halisi ambae kila timu inatamani iwe na mchezaji wa aina yake. Ni mrefu na hilo linamsaidia kucheza mipira yote ya juu inayokuja upande wake, ana nguvu pia ana akili kubwa ya kusoma njia za mpira, hivyo anakua na uwezo mzuri wa kukisia uelekeo wa mpira, na kufanya iwe rahisi kukutana nao na kuunasa au kuharibu pale inapobidi.
ANTHONY MATOGORO (KULIA) AKIWA NA KOCHA MSAIDIZI WA MBEYA CITY MAKA MWALWISI

        Siku walipocheza na Azam jijini Dar, alimpa wakati mgumu mno  Humphrey Mieno, kwani alikua akivuruga kila mpango uliokua ukitaka kutengenezwa, na hata walipocheza na Simba Dar , alicheza wa kiwango cha juu sana kiasi kipindi cha pili chote Amri Kiemba alipotea na hakua na madhara yoyote.  Katika mchezo na Yanga Dar, alitembea muda wote wa mchezo na Haruna Niyonzima, na kumfanya kila mara awe anagombana na mwamuzi. 
         Ana uwezo wa kucheza namba zote za nyuma, pia ana akili sana ya kugawa mipira hata katika nafasi ndogo, hivyo muda mwingi wa mchezo hua anafanya maamuzi ambayo ni sahihi na magumu  kwa mtu anaekabana nae.
ANTHONY MATOGORO(no16) AKIWA NA KIKOSI CHA MBEYA CITY
       Anthony Matogoro alizaliwa Mwanza na kusoma huko huko Mwanza na alianza kucheza soka akiwa na marafiki zake katika  timu ya mtaani ya  Kambarage iliyopo Mwanza,  baadae viongozi wa timu ya Pamba wakamuona na kuvutiwa na  kipaji chake hivyo wakamchukua, akachezea timu hiyo katika ligi daraja la kwanza na mwaka 2011 kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi akamchukua na kua ni miongoni mwa wachezaji walioipandisha hadi ligi kuu.
MATOGORO  AKIWA MAZOEZINI
    Akiongelea timu yake ya Mbeya City, anasema ana furaha  kucheza katika timu hiyo kwani ni kama timu ya familia moja, na kocha wao Juma Mwambusi ni sawa sawa na mzazi wao  “Tunafurahia sana kucheza chini ya kocha Mwambusi, kwani anatufanya kama ni familia moja na kutupa hamasa wachezaji wote kiasi hata yule ambae hajapangwa anajiona kama vile nae yumo ndani anacheza, anajituma katika kutufundisha na hata ukikosea ni mwepesi wa kukukumbusha wajibu wako” alisema Matogoro.
      “ Pia kitu kingine kikubwa kinachotufanya tufanikiwe ni sapoti kubwa na mshikamano wa mashabiki wetu, hua tunajisikia tuna amani kwa hamasa inayoletwa na mashabiki kila mahali tulipokwenda kucheza, sidhani kama itakuja tokea mashabiki wakaipenda timu yao hapa Tanzania kama ilivyo kwa hawa wa Mbeya City, tunawashukuru sana na tuko nao kuhakikisha tunafanya vizuri katika michezo yetu yote iliyo mbele yetu” alimalizia.
   

      

No comments:

Post a Comment