Friday, 21 February 2014

Tz prisons kamili kuwavaa azam

   Kikosi cha Tz Prisons kipo tayari kupambana na timu ya Azam wikiendi hii katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Mchezo huo utafanyika katika uwanja wa Azam Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar.

        Tz Prisons toka mzunguko wa pili uanze imeonyesha dhamira ya  kufanya kweli,  kwani katika michezo minne iliyocheza imeshinda mitatu na kutoka sare mmoja, na mchezo wa mwisho waliweza kuwafunga Ruvu Stars kwa mabao sita kwa bila hivyo huonyesha ni kwa jinsi gani walivyo katika moto muda huu.
       Akiongelea kuhusu mchezo huo, kaimu msemaji wa timu hiyo Junior Matukuta amesema timu yake iko vizuri na  wachezaji wana ari kubwa sana kwa mchezo wa kesho na michezo mingine inayokuja. “Katika mzunguko wa kwanza timu ilikua ikicheza vizuri sana lakini bahati haikua yetu, utaona mwenyewe kila mchezo tulikua tukicheza kwa kiwango kikubwa lakini mwisho hatupati matokeo mazuri, ila kwa sasa hivi tuko sawa na tuna uhakika wa kushinda michezo mingi ijayo” alisema Matukuta.
         “Azam ni moja ya timu nzuri hapa nchini na sisi pia ni wazuri na tupo katika ligi muda mrefu, hivyo hatuna wasiwasi na mchezo huo” aliongeza Mtukuta.
    Katika michezo yake ya karibuni, wamefanikiwa kutoka sare na Coastal Union ya bila kufungana, wakaifunga Ruvu Shooting magoli matatu kwa moja, wakaifunga Mtibwa moja bila  na kisha mchezo wa mwisho wameifunga  Ruvu Stars kwa magoli sita kwa bila.
     Wachezaji wote wapo katika hali nzuri na hadi sasa hakuna majeruhi yeyote.

             MUNGU IBARIKI TZ PRISONS…….

No comments:

Post a Comment