Mbeya city tunasonga mbele
Timu ya Mbeya City,imepoteza mchezo
wake wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania baada ya kufungwa goli moja kwa bila na Yanga katika
mchezo uliochezwa jumapili.
Goli pekee lilifungwa na Mrisho
Ngasa baada ya kukutana na mpira wa krosi krosi uliookolewa kwa kichwa na beki wa City
Yusuf Abdallah na kumkuta Ngasa aliyeusogeza na kupiga kiki iliyoingia pembeni mwa goli laMbeya City.
Katika mchezo huo Mbeya City walijitahidi kutafuta goli la kusawazisha lakini ilikua ni ngumu sana kwani kwa muda wote wa
kipindi cha pili kuanzia dakikaya 47 walicheza pungufu baada ya kiungo wao mzoefu
Steven Mazanda kutolewa kwa kadi nyekundu na mwamuzi wa pambano hilo.
Baada ya mchezo,kocha watimu ya Mbeya City
Juma Mwambusi alisema timu yake ilifungwa kutokana na kucheza pungufu kitu
ambacho ni kigumu sana kwa timu yoyote ya hapaTanzania ukichukulia unacheza na timu kama Yanga lakini akasema hayo
yamepita sasa hivi wanatazama mchezo unaofuata, kwani vita bado sana kuimaliza.
Akiongelea
kadi aliyopewa Mazanda, kocha Mwambusi alisema “mwamuzi ilitakiwa
amuonye, kwani tayari alikua na kadi ya njano,kawaida mwamuzi anatakiwa
amwambie kwamba hili ni onyo la mwisho,ukirudia tena utapata kadi
nyekundu,lakini yeye aliitoa moja kwa moja kama vile alikua akisubiri afanye
hicho kitendo ili amtoe, lakini huo ndio mpira wetu na hao ndo waamuzi wetu,
sitaki kabisa kulalamika kuhusu maamuzi yake kwani nitakua najirudisha nyuma,yaliyotokea tayari yametokea
tunasonga mbele”
Kwa ujumla timu ilicheza vizuri vipindi
vyote viwili, ingawa alipotolewa Mazanda mipango ikabidi ibadilishwe. Deus Kaseke
anayeshambulia kupitia pembeni kushoto , ikabidi aingie katikati
kusaidia viungo, hivyo kumfanya Hassan Mwasapili aliyezoea kukaba na
kushambulia acheze sana nyuma ili aweze kuwadhibiti Ngasa na Msuva. Ukichukulia
mashambulizi mengi ya Mbeya City hua yanaanzia upande wa kushoto, hali hiyo
iliathiri kidogo mashambulizi mengi kuelekea golini mwa Yanga.
Kwa wachezaji mmoja mmoja kila mmoja
alijitahidi sana kucheza kwa uwezo wake wote, ingawa beki
Yusuf Abdallah ndio alikua nyota upande wa
Mbeya City, kwani aliweza kuwamudu vilivyo washambuliaji wa Yanga.
Ukitazama mchezaji mmoja mmoja utaona kila
moja alitimiza majukumu yake kama alivyopangiwa..
- David Buruan alionyesha ukomavu wake kwani
mara kadhaa aliokoa hatari na alikua akiwapanga mno mabeki wake…..
- John Kabanda aliweza kumzuia sana David Luhende ingawa
krosi iliyokuja kuzaa goli ilitokea upande wake lakini si kwamba alikua kakosea
ni bahati mbaya beki aliyekuja kuosha mpira ukamkuta Ngasa. Kabanda alipiga krosi
kadhaa langoni mwa Yanga ingawa hazikuzaa magoli.ila alicheza vizuri sana.
- Hassan Mwasapili kama kawaida alicheza
vizuri sana ingawa kadi aliyopewa Mazanda ilimuathiri zaidi yeye kwani mara
nyingi yeye pamoja na Deus Kaseke wamezoea kushambulia na kukaba kwa pamoja,
hivyo Kaseke alipoingia katikati kazi
kubwa aliifanya peke yake, alifanikiwa kwa kiasi kikubwa.
-Deogratius Deo Julius alicheza
kwa utulivu wa hali ya juu, kwani alimficha muda mwingi wa mchezo Didier
Kavumbagu, na hakua na papara wakati wa kuokoa hatari nyingi zilizokuja langoni
mwa Mbeya City.
-Yusuf Abdallah, kwangu mimi
naona alikua ni nyota wa mchezo upande wa City, alikua na timing nzuri za
kuokoa mipira na mara nyingi alikaa mbele ya washambuliaji wa Yanga kila mpira
unapopigwa kuelekea golini mwa City. Aliiwahi mipira mingi na alifanya “tackling”
nyingi zenye mafanikio, pia alicheza mipira mingi sana ya juu…. Kiujumla alikua nyota .
-Anton Matogolo alipakamata
katikati , ingawa dakika za mwanzo alikua taratibu sana lakini baadae
alibadilika na alipotolewa Mazanda alifanya kazi kubwa sana ya kunyang’anya
mipira na kupiga pasi ndefu nyingi…nadhani aliongoza upande wa City kwa kupiga
pasi nyingi.alikua anajua timing za kuwafata kina Domayo na Niliyonzima.
-Peter Mapunda ni mmoja wa hazina
za Mbeya City, kwani aliweza kuipenyeza mipira kila mara kwa washambuliaji wa
katikati. Ana kasi na pia anapiga chenga huku akimfata beki…..uko vizuri sana
Peter..
-Steven Mazanda- nadhani mwamuzi
alimchagua mtu wa kumpa kadi nyekundu, kwani
Mazanda alikua akitoa pasi na kuwatuliza viungo wa Yanga. Ukitazama toka
mpira unaanza hadi anatolewa alipoteza pasi si zaidi ya mbili, na alikua kila
mara anaigawa mipira katika njia ambazo ni ngumu kutokufika.mwamuzi alifanya
kitu kibaya sana kumtoa mtaalamu huyu.
-Paul Nonga alikua akiwasumbua
sana mabeki wa Yanga, alikimbizana nao na pia alikua akiisogeza mipira
anakotaka ingawa nae aliathirika sana na kutoka kwa Mazanda.
- Mwagane Yeya-siogopi kusema
kwamba huyu ndie mshambuliaji wa kweli Tanzania. Nadir Haroub na Kelvin Yondani hawakwenda mbele hata mara
moja kama ilivyo kawida yao katika michezo mingine, walitulia na kujaribu
kumdhibiti ingawa ilikua ni kazi ngumu sana. Aliicheza mipira yote ya juu na
alikua ni tishio kila anapoupata mpira,
ni kwa vile bado alikua hajapona vizuri majeraha yake ndio maana kocha akamtoa
kipindi cha pili mwishoni na kuwapa ahueni mashabiki na walinzi wa Yanga. Anajua
sana huyu ticha.
-Deus Kaseke – nadhani mwenye
jibu zuri la jinsi Kaseke alivyocheza ni Mbuyu Twite, kwani alisumbuliwa sana na sikushangaa kocha anamtoa na kumuingiza JumaAbdul, Deus alikua
akimtoka Twite na mabeki wenzake kama anavyotaka. Ni mmoja kati ya vipaji adimu
sana hapa Tanzania. Kila mara anatia njaa na kuwafanya mabeki wa Yanga
kulaumiana muda mwingi wa mchezo. Hali ilibadilika kidogo alipoingia katikati
kwani ikabidi acheze kwa nguvu sana ili kuweza kuhimili viungo wa Yanga lakini
kwa ujumla alimudu sana kazi hiyo.
Waliokuja kuingia Saad Kipanga, Richard Peter na Yusuf Wilson
nao walicheza vizuri mno ingawa hawakupata muda mrefu lakini ki ujumla hii
inaonyesha Mbeya City ina wachezaji wengi sana wenye viwango vinavyolingana…
Kwa sasa hivi timu inasonga mbele na
kusubiri mchezo unaokuja…..




No comments:
Post a Comment