Thursday, 6 February 2014

WATAALAMWA KUPUNGUZA NA KUJENGA MWILI
GOLD GYM MBEYA

Ni kazi rahisi sana kunenepa na kuharibu shepu yako, lakini ni vigumu mno kuondoa huo unene. Watu wengi wanatumia gharama kubwa ili kujaribu kupunguza mwili ulioongezeka bila ya kupenda.

     Fikiria, unaamka asubuhi,unakula kisha unapanda gari na kwenda kazini, ukifika unakaa mezani, unaletewa chai  au wengine hata supu, unakula unafanya kazi kisha mchana unaenda lunch, na baadae jioni unapanda gari unarudi nyumbani. Unakua hujaushughulisha mwili kwa lolote, bila ya kujijua unaongeza mwili wako na hadi uje kustuka unakua tayari umechelewa.
   UNAKUA  huwezi kuvaa nguo za kukupendeza kwani tumbo litaonekana ni kubwa, unakua unaogopa hata kujitazama katika kioo kwani unaona wewe sio yule wa zamani uliyemzoea.
     Kuna wanaojaribu kufanya mazoezi ili wapungue, kuna wale wanaopunguza kula (diet) lakini inakua ni ngumu sana kufikia malengo, na kuna wale ambao kila siku anatoa ahadi kwamba kesho ataanza mazoezi ili apungue au kesho ataanza kujinyima kula ili apungue, lakini inakua ngumu, kesho inakua kesho na kesho yenyewe haifiki na mwili unazidi kuongezeka.
        Yusuf Chiba anamiliki sehemu ya kufanyia mazoezi katika eneo la uwanja wa Sokoine jijini Mbeya,inayoitwa GOLD GYM ana utaalamu wa muda mrefu kuhusu jinsi ya kuutunza mwili  na kuuweka katika shepu unayoitaka.
     Anasema kuna njia nyingi sana za kukufanya upunguze mwili wako “kwanza elewa kitambi au unene  unatengenezwa na chakula ambacho umekula na hakijafanya kazi mwilini, yaani ni chakula ulichozidisha kula, hivyo kinapokua mwilini hua mara nyingi kinakimbilia au tumboni au katika wowowo, ndio maana utaona watu wengi wakiridhika na kula vizuri basi lazima ananenepa, pia unapokula sana vyakula vyenye mafuta ni vigumu sana kusagika hivyo vinazunguka na kujikuta vimekaa tumbon na kukufanya uwe mnene  na kitambi”
       “Ili upunguze kitambi au unene inabidi uyeyushe hayo mafuta na njia ya kuyeyusha kubwa ni kufanya mazoezi, na inatakiwa ufanye mazoezi kwa kufuata masharti na sio kufanya tu ili uonekane unafanya mazoezi,  kwa mfano, kuna watu wanafanya sana mazoezi lakini akimaliza anakula chakula kingi na chenye mafuta na  anakunywa  juice nyingi yenye sukari ambayo humuongezea vile alivyopoteza anapofanya mazoezi! Si mara moja au mbili nimeona mtu akitoka kufanya mazoezi anaenda kupumzika bar na kunywa bia, hivyo inakua haimsaidii kupunguza mwili bali inamuongeza tu pumzi na kumuweka fit lakini unene unabaki pale pale” anasema Chiba.
        Kwa vile tumekubaliana unene unasababishwa na chakula ambacho umekula na hakifanyi kazi, nitajaribu kukupa njia rahisi za kuweza kukusaidia kupunguza unene na kitambi, ni rahisi sana kwa kuzisoma lakini utekelezaji wake ni mgumu kwa vile inatakiwa nidhamu ya hali ya juu sana. Lakini kwa vile una nia ya kupunguza  mwili wako hebu jaribu njia hii ;
           CHAKULA-
1-Epuka sana kula chakula chenye mafuta au kinachokaangwa na mafuta, kwani ni vigumu sana kuyeyuka kinapofika mwilini.
2- kula ili ushibe tu si kula sana kwa vile chakula kipo.
3-punguza sana kunywa soda na juice pamoja na bia
4-kua active usikae sana sehemu moja,jaribu angalau kutembea tembea.
5-fanya mazoezi kila siku.
        NAMNA NZURI YA KUPUNGUZA MWILI
Wengi hua wanajarubu kufanya mazoezi ya tumbo ili kulipunguza, lakini hilo ni kosa kubwa sana kwani unapofanya mazoezi ya tumbo unalifanya liwe gumu na lina nguvu lakini kupungua ni sifuri!!!wengi hawaelewi hilo jambo lakini mazoezi mengi ya tumbo ni kulifanya liwe strong sio kulipunguza.
Nitakupa njia ya kufanya hayo mazoezi ukichanganya na diet rahisi ili upungue.
1.     TUKIANZIA katika chakula, chunguza kwa siku unakula kiasi gani kwa kila mlo, mfano kila asubuhi unakunywa chai vikombe viwili, chapati mbili, sambusa mbili,juice au soda na glass ya maji. UNACHOTAKIWA KUFANYA
-kwa wiki ya kwanza punguza nusu ya unachokula, hivyo asubuhi kunywa chai kikombe kimoja,chapatti moja,sambusa moja, usinywe juce au soda, kunywa na maji.
-mchana pia punguza kiasi cha chakula unachokula kiwe nusu ya unachokula kila siku.nadhani mwenyewe unajua kipimo cha chakula unachokula.
-usiku pia fanya hivyo hivyo, najua ni vigumu sana lakini nina uhakika na matokeo yake.
   MAZOEZI- kwanza hakikisha umepima una kilo ngapi kabla ya kuanza mazoezi.
  -Kila siku fanya mazoezi mara mbili kwa siku kwa njia ifuatayo
Iwapo hujafanya mazoezi muda mrefu anza taratibu.
 Tafuta kamba ya kuruka na ukiamka tu jambo la kwanza anza kuruka kamba na njia yake ni kama ifuatavyo.
Wiki ya kwanza  ruka mara 30 kisha unapumzika dakika moja, unaruka tena mara 30 unapumzika dakika moja hadi ufike round 10,kwa maana hiyo utakua umeruka mara 300. Yaani 30 x10. Kisha ukimaliza kuruka jitahidi upige push up hata mara 15 kisha kaoge  ndio unywe chai. Na chai inatakiwa unywe kama nilivyoelekeza hapo juu.
Jioni kabla ya kula rudia tena hayo mazoezi kwa njia ambayo nimekuelekeza , fanya hivyo wiki nzima na kula kama nilivyoelekeza kwa wiki nzima. Baada ya wiki utakua umeanza kuzoea hapo unaongeza tena badala ya kuruka mara 30, unaruka mara 50 x 10 iakua ni mara 500. Na hakikisha unapumzika kwa dakika moja tu usizidishe maana ni muhimu sana kuufanya mwili usipoe.
MUHIMU- hakikisha unakula saa moja au dakika 45 kabla ya kulala ili chakula ulichokula kifanye kazi, ni mbaya kula kisha unalala,maana hapo chakula kinakua hakijafanya kazi yake na kinageuka kua ni ziada.

       WIKI ya tatu punguza tena chakula kidogo ya kile unachokula, vizuri zaidi kama ukipunguza tena nusu ya unachokula  wakati huo, hivyo ina maana itakua ni robo ya chakula ulichozoea kula kila siku, Najua ni ngumu mno kufanya hivyo lakini nakuhakikishia ukija kuzoea utaona ni jambo la kawaida kabisa.
 Na hakikisha unaendelea na mazoezi kila siku bila kufanya uvivu,  utakapojiona unazidi kupata pumzi ongeza lap za kuruka hadi ufike mara 100 au hata 150, ina maana kila chakula ulichokula kitakua kinatumika na pia utakua unaunguza na mafuta yaliyopo mwilini mwako. Baada ya mwezi nina uhakika utakua umepungua kwa kiasi kikubwa sana.
    Usisahau kupima uzito kila mara ili uone ni kwa kiasi gani unapungua.
       KWA WALE WALIOPO JIJNI MBEYA AU WANAOTAKA KUJUA ZAIDI JINSI YA KUFANYA ILI KPUNGUZA MWILI  WAWASILIANE NA YUSUF CHIBA KWA NAMBA YA SIMU  0659 464 344



No comments:

Post a Comment