David buruan;
Kila mchezo unaokuja ni fainali
Kipa wa timu ya soka ya Mbeya
City ya jijini Mbeya, David Buruan amesema sasa hivi wanajipanga ili kila
mchezo watakaocheza uwe kama ni fainali, hivyo wapo makini sana kuhakikisha
wanapata pointi tatu katika kila mchezo.
“Kwa sasa hivi timu yetu pamoja na
uchanga wake, imekua ni kama zile timu
mbili kubwa zinazojulikana hapa nchini, kila tunakokwenda tunakuta timu
zimepania ili kuweza kutufunga, hivyo na sisi tumeamua tusibweteke , tufanye kazi zaidi ya mwanzo ili kuhakikisha tunafanya vizuri” alisema
kipa huyo.
“Miaka iliyopita, timu zilikua
zikiwekwa kambini pale tu zinapotaka
kucheza na Simba au Yanga, na hata Simba na Yanga zilikua zikiweka kambi pale tu
zinapotaka kukutana zenyewe, lakini kwa sasa ni tofauti, hata Yanga pamoja
na kua walikua na kambi nzuri nje ya nchi. Lakini walipokaribia kucheza nasi
wakaweka tena kambi Bagamoyo, hiyo
inadhihirisha kwamba wanatuchukulia kwa
tahadhari kubwa, na sisi inabidi
tuzidishe juhudi zaidi ya zile za siku za nyuma” aliongeza David Buruani ambae
msimu uliopita ndio alikua kipa bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania.
“Kila mmoja katika timu yetu
anajua wajibu wake, hivyo ni rahisi kufikia malengo pale tunapojiwekea na kwa
sasa hivi malengo yetu ni kuhakikisha hatupotezi pointi katika michezo
inayokuja” aliongeza David.
Kuhusu mchezo na Yanga walipoteza kwa
goli moja anasema “ ule mchezo umepita, nashukuru wachezaji wote wamekwishasahau kuhusu huo mchezo,
wamehamisha akili zote katika hii mingine nayokuja mbele, tunaomba Mungu atusaidie
tukichanganya na juhudi zetu tuna uhakika tutafika mahali ambapo tunataka kufika”alisema.
Na kuhusu mashabiki wa Mbeya City akasema
“Sio siri. Mafanikio yetu kwa asilimia kubwa yanaletwa kutokana na hamasa inayoonyeshwa na mashabiki
wetu, wanatufuata kila tunapokwenda na hilo halijawahi kutokea katika hizi nchi
za Africa, kwetu sisi tunaona kama ni deni na kulipa kwake ni kujituma ili
kupata ushindi. Hua naona raha sana kila ninapokua uwanjani nikitazama nje
mashabiki wa timu yetu wanakua wamewameza mashabiki wa timu pinzani….mfano
uliona siku tumecheza na Azam na pia siku tumecheza na Yanga, ilikua kama tuko nyumbani uwanja wa Sokoine, mashabiki walikua
wanashangilia kuanzia mwanzo wa mchezo hadi mwisho na kutufanya tupate ujasiri
zaidi wa kupambana, tunawashukuru sana
mashabiki wetu, tutajitahidi tusiwaangushe” alimalizia David Buruani.
picha zote kwa hisani ya David Baruan.imeandikwa na Abdul Sudi,Mbeya.





No comments:
Post a Comment