Wednesday, 12 February 2014

Peter mapunda
BUNDUKI YA MBEYA CITY

         Imeandikwa na Abdul Sudi, Mbeya/picha kwa hisani ya www.bayana.blogspot na Peter Mapunda.
             Mbeya City ina washambuliaji wengi,  na kila mmoja akipata nafasi anaitumia. Wengi tunamfahamu Mwegane Yeya, ana magoli matano tayari katika ligi kuu na matatu kati ya hayo aliwafunga Azam, tunamfahamu Paul Nonga, Jeremiah John na hata Richard Peter, pia tunawafahamu kina Deus Kaseke, Mohamed Kijuso na Alex Seth, wote wana uwezo mkubwa sana.

       Peter Mapunda alipata nafasi ya kucheza siku walipopambana  na JKT Oljoro, akafunga na walipotoka pale wakaelekea Tabora kucheza na Rhino huko nako akafunga kisha wakacheza na Tz Prisons pia  akafunga na juzi tena amewafunga Mtibwa, hiyo ni kudhihirisha kwamba ana uwezo mkubwa sana wa kufunga.
PETER MAPUNDA AKIMTOKA MBUYU TWITE WA YANGA.
     Alizaliwa Songea na kupata elimu yake huko huko Songea na alianza kucheza mpira katika timu ya mtaani iliyokua ikijulikana kama Majengo Sports. Na hapo viongozi wa timu ya Polisi wakamuona na kumchukua ambapo alishiriki lig daraja la tatu kabla hajachukuliwa na timu kongwe ya Maji Maji ya huko huko Ruvuma.
      Baadae kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi akamuona na kuvutiwa na kipai chake na kuamua kumchukua, ambappo hadi sasa ni mmoja wa wafungaji tegemezi wa Mbeya City.
    Ana kasi na pia anapiga chenga, ana uwezo wa kupiga miguu yote miwili,  na ana uwezo wa kushambulia kutokea katikati au hata pembeni.Na kikubwa magoli yake anafunga kwa njia tofauti, kwa kichwa au hata kwa miguu yote miwili, wa kushoto na kulia, hivyo kumfanya aweze kufunga hata katika mazingira magumu.
PETER MAPUNDA AKIMSUMBUA NADIR HAROUB.
      Akiongelea siri ya mafanikio ya timu hiyo, peter anasema “kikubwa ni kwamba kila mchezaji aliye Mbeya City ana uwezo na anastahili kuwepo hapa, hivyo akipata nafasi hua anaitumia kwa uwezo wake wote, ndio maana huoni kama kuna tofauti mchezaji mmoja akitoka na kuingia mwingine, pia mashabiki wetu wanatupa sapoti kubwa sana kila tunapocheza, wanasafir na sisi na kutufanya tujione kila mchezo kama vile tuko nyumbani, kiufupi Mbeya haina uwanja wa ugenini, viwanja vyote ni vya nyumbani”
PETER MAPUNDA AKIWA JUMA ABDUL.

      Pia hakuacha kumuongelea kocha Juma Mwambusi “ ni kocha tofauti sana kwani anatufanya wachezaji wote tujione kama ni familia moja, habagui mtu na hana mazengwe kama walivyo makocha wengine wengi tunaowasikia, ukikosea anakuambia kosa lako na maisha yanaendelea, ki ufupi ni kocha bora sana hapa nchini”. Alimalizia Peter.

No comments:

Post a Comment