Mbeya city;
Ni sisi na simba
Timu ya soka ya Mbeya City iko
tayari kuikabili timu kongwe ya Simba, katika mchezo unaotegemewa kua mkali na
wa kuvutia utakaochezwa jumamosi.
Akiongea kuhusu mchezo huo, kocha wa
timu ya Mbeya City Juma Mwambusi anasema vijana wake wapo tayari kwa mchezo
huo.
“Nashukuru mungu wachezaji wangu wote wapo
salama, hata wale waliokua majeruhi sasa hivi wamepona hivyo kunifanya niwe na
wigo mpana wa kuchagua watakaocheza, hata wale waliokua na adhabu za kadi kama
Steven Mazanda na Hassan Mwasapili, tayari wamemaliza adhabu zao na hivyo wanategemewa
kuanza katika mchezo huo” alisema.
![]() |
| kocha juma mwambusi |
Na kuhusu timu yake mara nyingi
kufungwa goli la mapema alisema “tayari nimewajenga kisaikolojia hivyo sasa hiv
wanajua hakuna tena kusema tunasomana kimchezo, wanatakiwa wawe makini dakika
zote za mchezo, na hilo naamin watakua wamelielewa na watalifanyia kazi”aliongeza.
Akiongelea mchezo huo beki wa kulia wa Mbeya
City John Kabanda alisema “ tunaamini kila kitu, kitakwenda
sawa, kwani tumefanya matayarisho mazuri ya ki mwili na kiakili hivyo
kilichobaki ni kwenda kufanya kazi, tunajiamini tutashinda huo mchezo na kukaa
kileleni mwa ligi hiyo”alisema .
![]() |
| yohana morris |
Nae Yohana Morris alisema “ki mpira na ki akili tupo vizuri sana, tunakwenda kupigana
ili tushinde, tulishasahau kuhusu timu kubwa na majina makubwa, tunaenda
kupambana vitani na kwa matayrisho tuliyofanya tuna uhakika tutashinda”
KILA LA KHERI MBEYA CITY…




No comments:
Post a Comment