Saturday, 15 February 2014

Mbeya city sare na simba

 Mbeya City imefanikiwa kutoka sare ya goli moja kwa moja na timu kongwe na ngumu ya Simba katika mchezo mzuri uliochezwa katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

            Katika mchezo huo, city walikua wa kwanza kupata bao lililopatikana kwa njia ya penati baada ya  Wiliam Lucien wa  Simba kuushika mpira  ndani ya eneo la hatari.
     Penati hiyo ilipigwa kiufundi na beki Deogratius Julius na kumfanya kipa wa Simba Beko asiwe na la kufanya.
KIKOSI CHA SIMBA KIKIINGIA UWANJANI.

     Mbeya City walimchezesha beki wake wa kushoto Hassan Mwasapili kama mshambuliaji na Hamad Kibopile kama mlinzi wa kushoto,  ambae alicheza vizuri sana hadi alipopewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi Singano hivyo ikambidi kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi afanye mabadiliko ili kumuepusha na kadi nyekundu na nafasi yake ikachukuliwa na Mwagane Yeya.

        City waliutawala  mchezo kipindi cha kwanza na Simba wakautawala zaidi kipindi cha pili.
KIKOSI CHA MBEYA CITY KIKIINGIA.

   Simba walipata bao la kusawazisha kupitia kwa mshambuliaji wake hatari  Amis Tambwe mwanzoni mwa kipindi cha pili baada ya kupata mpira toka kwa Haruna Chanongo.
MASHABIKI  WAKILANGULIWA TIKETIA

     Tiketi za mchezo huo zilikwisha mapemasana kiasi umati mkubwa wa watu ulibaki nje baada ya kukosa tiketi na walanguzi waliweza kulangua tiketi hizo hadi kufikia shilingi 15000 na 20000.

No comments:

Post a Comment