Real yainyoa barca
Real Madrid imeifunga Barcelona
na kuweza kuchukua kombe la mfalme, katika mchezo huo Real ilishinda kwa magoli
mawili kwa moja.
Huu unaweza kua ni msimu wa kwanza kwa
Barcelona kumaliza msimu bila ya kombe lolote kwani tayari wametolewa katika
kombe la Ulaya na pia wapo katika hati
hati ya kupata ubingwa wa La Liga.
Marid walikuwa wa kwanza kupata goli
lililofungwa na Angel Di Maria baada ya Barcelona kufanya shambulizi na wakapoteza
mpira na Luca Modric akampa Bale ambae aliupeleka haraka kwa Isco aliyempa Di
Maria na huku Barcelona wakidhani ameotea, aliweza kumchambua kirahisi kipa wa
Barcelona Pinto na kuandika bao la kwanza.
Goli hilo lilizidi kuonyesha kwamba
timu ya Barcelona ukuta wake ni dhaifu hasa kutokana na kua majeruhi kwa
wachezaji kwa Carlos Puyol na Gerard Pique.
Barcelona walisawazisha katika dakika
ya 68, bao hilo lilifungwa kwa kichwa na Bartra kufuatia kona iliyopigwa na Xavi.
Goli la pili la aMadrid lilipatikana tena
kwa shambulizi la kustukiza baada ya Barcelona kushambulia na walipopoteza
mpira na Bale akaupata nyuma ya katikati
ya uwanja, akamzidi mbio beki wa Barca Coentrao, na kisha akamzidi ujanja kipa
Pinto na kuupitisha mpira katikati ya miguu ya kipa huyo.
Lilikua ni goli zuri sana lililowafanya
Madrid kutwaa kombe la mfalme.





No comments:
Post a Comment