Wednesday, 23 April 2014

ATLETICO SARE NA CHELSEA

Atletico Madrid  wametoka sare ya bila kufungana na Chelsea  katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali wa klabu bingwa ya Ulaya katika uwanja wa Estadio Vicente Calderon.

   Matokeo hayo yamewafanya Chelsea angalau kua na matumaini ya kupita kwa vile mchezo ujao watacheza katika uwanja wa nyumbani.

       Kocha wa Chelsea atakua na wakati mgumu wa kupanga kikosi chake kwani kipa wa timu hiyo Petr Cech aliumia  baada ya kugongana na mchezaji wa Atletico katika kipindi cha kwanza, na baadae kipindi cha pili kapteni wa timu hiyo John Terry nae alitolewa baada ya kuumizwa na mchezaji mwenzake David Luiz.

     
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho alisema “Petr Cech hatacheza tena msimu huu lakini John Terryatakuwepo ikiwa tutafanikiwa kufika fainali”.

       Ingawa Chelsea watakua na faida ya kucheza mchezo wa pili nyumbani, lakini Atletico Madrid wana rekodi nzuri ya kushinda ugenini, kwani walikwishawafunga Ac Milan, na Porto ugenini kisha waliweza kutoka sare na timu ngumu na nzuri ya Barcelona ugenini.

    Nae kocha wa Atletico Diego Simeone alisema kila timu imejaribu kucheza kwa ubora ilioona unafaa, ingawa Chelsea walilinda sana lango lao, hilo tulilitegemeakwani kwa vile wanacheza ugenini waliona silaha kubwa ni kulinda. Matokeo haya yanaufanya mchezo kua wazi kwni kwa vile wao kwao lazima wafunge itatakiwa watushambulie na sisi hao ndipo tutapata nafasi ya kucheza mchezo wetu tuliozoea.

      Chelsea ambao wapo katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya Uingereza, pointi tano nyuma ya wanaoongoza Liverpool,wana nafasi ya kupunguza hizo pointi,  kwani jumapili watakutana.
   Frank Lampard alipona kupata kadi baada ya kuugonga kwa makusudi mpira uliokua umepigwa na mchezaji wa Atletico.

     Mourinho alisema na michezo miwili migumu, wa Liverpool jumapilia na baadae jumatano wa Atletico, hivyo anatamani achezeshe wachezaji ambao hatawatumia jumatano siku anacheza na Liverpool.
    Katika mchezo huo, Atletico walitawala sehemu kubwa sana ya mchezo, lakini mabeki na viungo wa Chelsea walikaba vizuri sana  na kufanikiwa kuokoa hatari zote zilizoelekezwa katika lango lao.



No comments:

Post a Comment