Thursday, 24 April 2014

Real yaifunga bayern

Real Madrid imefanikiwa kuwafunga Bayern Munich 1-0, katika ligi ya mabingwa Ulaya mchezo ambao Bayern waliutawala kwa muda wote.

   Goli pekee katika mchezo huo lilipatikana kipindi cha kwanza likiwekwa wavuni na Karim Benzema katika dakika ya 19 baada ya kupata pasi toka kwa Coenrao.

   Ingawa Bayern waliumilii sana mchezo, lakini Real ndi waliopoteza nafasi nyingi za kufunga, kwani mara kadhaa walifika golini kwa mashambulizi ya kushtukiza lakini wakshindwa kufunga.

    Christiano Ronaldo ambae alicheza huku akitoka kaika majeruhi alipoteza nafasi mbili nzuri za kuweza kuwahakikishia ushindi.
   Gareh Bale aliingia mwishoni mwa kipindi cha pili akimbadili Ronaldo na akaleta uhai baada ya kupiga krosi kadhaa zilizoshindwa kumaliziwa na washambuliaji wa Bayern.

    Arjen roben alikua akiisumbua safu ya ulinzi ya Real, lakini mara zote waliweza kujipanga na kuondoa hatari nyingi alizokua akizileta.


No comments:

Post a Comment