MOYES
ATIMULIWAUNITED
Manchester United hatimaye
wameamua kuvunja mkataba na kocha wao David Moyes. Wamemteua Ryan Giggs kua kocha wa muda hadi msimu utakapokwisha.
Kipigo cha 2-0 toka kwa Everton ndio ilikua msumari
wa mwisho kwa Moyes, kwani timu haikucheza vizuri katika kila idara.
 |
| siku walipofungwa 1-0 na Liverpool |
Moyes aliteuliwa na Sir Alex Ferguson ili
amrithi baada ya kudumu kwa miaka 27 akiwa kocha wa United. Lakini Moyes amedumu
kwa miezi kumi tu!.
Mabingwa hao watetezi wako nafasi ya saba katika ligi, na watamaliza
ligi wakiwa na point chache kuliko miaka yote toka ligi kuu ianze.Kipigo cha
Everton kilikua ni cha 11 katika ligi msimu huu, na kwa mara ya kwanza toka
msimu wa 1995/96 watakosa kushiriki ligi ya mabingwa.
 |
| akiwa hajui la kufanya |
Ingawa Moyes mwenyewe kila mara alikua
akisema anapata sapoti ya uongozi na
hata mashabiki, lakini mwisho wa siku wamiliki wameona bora yaishe .
 |
| akilalamika kunyimwa penati na Tottenham |
Wiki iliyopita Moyes alitamka kwamba yupo
katika harakati za kufanya usajili makini, na alikua na matumaini ya kusajili
nyota kadhaa kabla ya kuanza kwa kombe la dunia, wachezaji kama beki wa kushoto
Luke Shaw waSouthamtpton na kiungo wa Sporting Lisbon William Cavalho walikua
katika list ya Moyes.
 |
| akiwa haamini kipigo toka kwa West Brom |
Baada ya kipigo cha Everton Moyes alisema “kila
mmoja anajua sasa hivi tupo katika mabadiliko,kuna mambo ambayo tupo njiani
kuyafanya”.
Wiki iliyopita wamiliki wa timu hiyo familia
ya Glazer walimwambia Moyes afanye kila analoweza ili angalau wapate nafasi
katika ligi ya Europa. Lakini hilo nalo lilikua shakani baada ya kipigo cha
Everton.sasa hivi United wapo point sita nyuma ya Tottenham ambao wako nafasi
ya sita na michezo iliyobaki ni minne tu.
 |
| shabiki akitaka kwenda kumvamia baada ya matokeo mabovu dhidi ya Man City Old Traford |
Manchester United wamepoteza kwa Liverpool,Manchester City na Everton
nyumbani na ugenini, hali iliyosababisha kufikia hata mashabiki kuanza kumlaumu
Ferguson kwa kumteua Moyes.
 |
| akiwa haelewi kipigo cha city Etihad |
Katika mchezo na Aston Villa, mashabiki
waliokua wanampinga Moyes walikodi ndege na kupeperusha bango lililokua
likimtaka Moyes aondoke katika timu hiyo.
 |
| akijaribu kukimbilia mpira ili aokoe muda dhidi ya Spurs |
Toka aanze kuifundisha United, Moyes
alifanikiwa kuifunga timu kubwa moja tu Arsenal, na aliweza kukusanya poini
sita tu toka kwa hizo timu kubwa. United pia walipata kiigo cha aibu nyumbani toka
kwa West Bromwich na Newcastle na baadae
wakatolewa katika Ligi ya mabingwa na Bayern Munich.Pia walitolewa katika kombe
laligi na Sunderland, kisha wakatolewa raundi ya tatu katika kombe la FA na
Swansea.
 |
| KWA HERI |
No comments:
Post a Comment