Tuesday, 29 April 2014

  Hamid mohamed
Mbeya city mpya

 Msimu wa ligi kuu ya vodacomTanzania umemalizia,na sasa hivi mambo yanayojadiliwa ni kuhusu usajili wa timu  zitakazoshiriki ligi hiyo msimu ujao. Moja ya timu hizo ni Mbeya City. Tofauti na timu nyingine, wenyewe wameamua kuwapandisha vijana wao waliokua timu B ili wakafanye kazi pamoja na kaka zao.
                  Mmoja wa vijana waliopandishwa katika timu hiyo ni Hamid Mohamed, anaecheza  kama  mshambuliaji wa pembeni. Na pia hata nafasi za katikati.
Hamid Mohamed
     Amezaliwa mkoani Mbeya na kusoma  katika shule ya msingi ya Magereza Kiwira, kisha sekondari akasoma shule ya Igawilo.
Alianza kucheza katika timu ndogo ya magereza Kiwira,kabla hajachukuliwa na timu ya Tz Prisons,
    Baadae mwaka  jana akajiunga na timu ya Mbeya City B. akashiriki mashindano ya Mufindi, kisha baadae  mwezi December akashriki katika mashindano ya Uhai Cup. Na muda wote huo alikua ni kapteni wa timu hiyo ya pili ya Mbeya City.
Hamid akiwa na Yohana Morris
  Baadae mwishoni mwa msimu uliomalizika,  kocha Juma Mwambusi akaamua kumpandisha na kua ni mchezaji wa timu ya kwanza ya timu hiyo.
   Na mchezo wake wa kwanza kucheza ligi kuu ni walipocheza na timu ya Mgambo jijini Mbeya na kuishinda kwa goli moja bila, alicheza kwa dakika 75 ndipo akabadilishwa na kuingizwa Jeremiah John.
        Kwa sasa hivi anaendelea na mazoezi akisubiri kwa hamu kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu.

  

       

No comments:

Post a Comment