Monday, 12 May 2014

NURDIN CHONA
BEKI WA KWELI BONGO

       Mshambuliaji aliyeongoza kwa kufunga magoli katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania, Amisi Tambwe hataki tena kukutana na  beki wa Tz Prisons, Nurdin Chona, kwani kwa jinsi alivyomzuia, hakua na ujanja wala njia ya kumpita japo mara  moja kwa dakika zote tisini walipocheza. Kila alipokwenda alijikuta Nurdin yupo nae,
akiruka kuufata mpira wanaruka pamoja,  ilifikia hadi wakaumia kichwani wote wawili katika jitihada za kuwania mpira,  Nurdin aliweza kuzuia njia zote kiasi kwamba Tambwe hakupata mipira mingi  na hakuweza kabisa kua na madhara. Hali hiyo pia ilimkuta aliyekua mshambuliaji mrefu wa Yanga Didier Kavumbagu, nae alipewa shughuli kiasi alipoulizwa baada ya mchezo hakusita kumtaja Nurdin kwamba ni beki imara na anaijua kazi yake.
NURDIN AKIPAMBANA NA SINGANO WASIMBA

         Nurdin mzaliwa wa Kigoma  amecheza karibu michezo yote waliyocheza Tz Prisons, ingawa mwanzoni hawakufanya vizuri lakini mzunguuko wa pili walikua vizuri sana. “Tulipoanza msimu uliokwisha timu ilikua vizuri, lakini hatukupata matokeo kutokana na mambo mengi, mojawapo ilikua ni maelekezo ya kocha hayakua yamekamilika. Lakini baadae alipokuja Kocha Mwamwaja hali ikabadilika, kwani kwanza alitujenga ki saikolojia kiasi wote tukajiona ni washindani na si wasindikizaji tena, na akatupa morali ya hali ya juu kiasi tukawa tunajiamini kwamba kila timu tutakayokutana nayo lazima tutaifunga, na ukweli tulifanikiwa kwa kiasi kikubwa” alisema Nurdin.
USO KWA USO NA NIYONZIMA
       Alianza kucheza mpira katika timu ya Nyika fc ya kigoma wakati huo akiwa anasoma na baadae mwaka 2012 akajiunga na timu ya Tz Prisons ambayo hadi sasa bado anaichezea. Ana nguvu na akili nyingi awapo uwanjani, hivyo kumpita inatakiwa ujipange na uwe mzuri sana.
        “Tz prisons  tuko vizuri na tumejipanga msimu ujao tushindane toka mwanzo hadi mwisho, yaliyotokea msimu huu hata sisi yametuumiza, lakini msimu ujao tunajipanga kufanya vizuri michezo yote, kwani bado tuna kikosi kizuri na wachezaji wenye uwezo mkubwa sana, tazama jinsi Jimy Shoji anavyoweza kumiliki katikati ya uwanja, naamini ni  kiungo bora Tanzania, hata Peter Michael ni mmoja kati ya wafungaji bora hapa Tanzania, na tuna wachezaji wengi wenye viwango vizuri na wanajua majukumu yao hivyo msimu ujao Tz Prisons itakua ni moja ya timu bora katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania.
AKIMZUIA JERRY TEGETEA
           Nurdin amecheza michezo 22 katika ligi iliyokwisha, hakucheza michezo minne tu walipocheza na Mgambo, Rhino na Kagera Sugar zote ugenini, na pia hakucheza siku walipokwaana na JKT Oljoro nyumbani uwanja wa Sokoine. “ Sasa hivi niko katika mazoezi makali nikijaribu kutengeneza nguvu ili msimu ujao nipambane  kikamilifu na washambuliaji nitakaokutana nao” alisema Nurdin.
HAPITI MTU
       “ninatamani sana siku moja nije kucheza soka katika ligi kubwa duniani, hivyo kila mara najitahidi kuongeza kiwango changu ili siku moja nije kua ni tegemeo la nchi yangu katika soka, ipo siku naamini haya yatatimia.”alimalizia Nurdin ambae timu kadhaa zimeanza kumnyemelea ili akachezee katika msimu ujao.

     

  

No comments:

Post a Comment