Ivo mapunda
KIPA ASIYECHUJA TANZANIA
Ukiongelea makipa bora kabisa waliowahi kutokea hapa nchini na bado wanatamba huwezi kuacha kumtaja Ivo Mapunda, pamoja na kua alianza kucheza mpira muda mrefu, lakini hadi sasa ubora wake unazidi kuongezeka. Ana uwezo wa kucheza mipira ya aina yote, ya juu na ya chini, pia umbo lake kubwa linamsaidia hata katika ile mipira ya kupambana na ya krosi
. kizuri zaidi ana uwezo mkubwa wa kucheza penati, na kikubwa anachowazidi makipa wengine ni jinsi anavyojua kuanzisha mashambulizi kila anapodaka mpira.
![]() |
| IVO MAPUNDA |
Si ajabu kuona mashabiki wa timu pinzani wakiwa na
wasiwasi kila anapokua golini, hua wanafikia hadi kuwaza kwamba taulo
analopenda kuliweka katika nyavu lina nguvu za giza,zinazomsaidia kulinda lango
lake. Ingawa ki ukweli ni imani zao tu
kwa kua mara nyingi wanashindwa kupata matokeo anapokua golini.
![]() |
| IVO AKIWA NA TAULO LAKE |
Ana uzoefu mkubwa sana, na kilichomsaidia ni kwamba alianza kucheza soka akiwa na umri mdogo hivyo amekutana na makipa na makocha wa aina nyingi katika timu tofauti alizochezea, amecheza ligi kubwa katika nchi
tatu tofauti na kwa mafanikio.
![]() |
| IVO MAPUNDA AKIWA NA SHAABAN KADO NA JUMA KASEJA |
Alizaliwa
katika sehemu inayoitwa Kisa Ushirika , Tukuyu Mbeya na kusoma katika shule ya
msingi hapo hapo Kisa aliposoma hadi darasa la sita akahamia Mafinga katika
shule ya Nyololo. Baadae akajiunga na shule ya
sekondari ya ufundi ya Ifunda. Na hapo
alichukua masomo ya motorvehicle mechanics, na alipomaliza alifaulu vizuri na
kuchaguliwa kwenda katika chuo cha ufundi Mtwara.
Hakuenda huko
chuoni, kwani muda huo tayari akili yake ilikua imezama katika soka.
Alirudi
nyumbani Mbeya na kuanza kucheza katika
madaraja ya chini, akianzia na timu ya Mpuguso Stars ya Ushirika Tukuyu.
Mfadhili wa
Tukuyu Stars wakati huo akiitwa Rampa alimchukua na kumpeleka Tukuyu Stars na
hapo alidumu miaka miwili kabla hajachukuliwa na timu ya Tz Prisons, na akawa
ni askari kamili wa jeshi la Magereza, akiwa na cheo cha koplo.
![]() |
| KOPLO IVOMAPUNDA |
Akiwa Tz Prisons
alikaa miaka sita kisha akahamia Moro United ya Morogoro. Hapo pia alikaa miaka
miwili na kuhamia katika timu ya Yanga.
Baada ya
miaka mitatu akaondoka katika timu hiyo na kwenda kuheza mpira a kulipwa katika
timu ya st George ya Ethiopia, kisha akarudi nyumbani Tanzania na kujiunga na
African Lyon ambapo pia alikaa miaka miwili na kisha akaamua kutoka tena na kwenda Kenya katika
timu ya Bandari Mombasa.
Alikaa
miezi sita na akachukuliwa na Gor Mahia
ya hapo hapo Kenya alikokaa miaka miwili, na ndipo klabu ya Simba ikaamua kumchukua na ndio anaitumikia hadi
sasa.
Akiongelea kuhusu soka Ivo alisema "kikubwa katika soka ni kujituma na kujaribu kujiepusha na mambo ambayo hayaendani na soka, ninashukuru nimecheza kwa muda mrefu kwa vile ninajua thamani yangu, hivyo ninajitunza na kufanya yale ambayo yanatakiwa kufanywa na mchezaji. Nimeanza kucheza nikiwa na umri mdogo sana, hivyo nimekutana na mambo mengi katika hii miaka niliyocheza. hakuna njia ya mkato, ni kufanya mazoezi kila siku hiyo ndio silaha ya mcheza soka."
" sasa hivi nipo Simba na matayarisho tunayofanya ni mazuri, hivyo na mategemeo yangu ni kwamba timu yetu itafanya vizuri zaidi kaitika msimu huu"
![]() |
| RAISI SHEIN WA ZANZIBAR AKISALIMIANA NA WACHEZAJI WA SIMBA KABLA YA MCHEZO NA KMKM |
Akiongelea kuhusu soka Ivo alisema "kikubwa katika soka ni kujituma na kujaribu kujiepusha na mambo ambayo hayaendani na soka, ninashukuru nimecheza kwa muda mrefu kwa vile ninajua thamani yangu, hivyo ninajitunza na kufanya yale ambayo yanatakiwa kufanywa na mchezaji. Nimeanza kucheza nikiwa na umri mdogo sana, hivyo nimekutana na mambo mengi katika hii miaka niliyocheza. hakuna njia ya mkato, ni kufanya mazoezi kila siku hiyo ndio silaha ya mcheza soka."
" sasa hivi nipo Simba na matayarisho tunayofanya ni mazuri, hivyo na mategemeo yangu ni kwamba timu yetu itafanya vizuri zaidi kaitika msimu huu"






No comments:
Post a Comment