Monday, 12 May 2014


 Uhuru selemani
 nashukuru nipo huru

            Sio siri, mmoja kati ya wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu hapa Tanzania ni Uhuru Selemani, ambae hadi msimu wa mwaka 2013/14 unamalizika alikua ni mchezaji wa timu kongwe ya Simba. Lakini sasa hivi ni mchezaji huru baada ya kukubaliana na timu hiyo kwamba hataweza kuongeza mkataba.
MAFANIKIO
     Uhuru mwenye uwezo wa kupiga miguu yote na ni jasiri asieogopa kupita katikati ya mabeki, alisema ameamua kutokuongeza mkataba ili apumzishe akili yake kutokana na presha ya kucheza katika mazingira magumu.
   “unajua kuna mambo mengi sana yanayofanyika katika hizi timu kubwa, mtu wa nje haelewi, mchezaji unajitahidi kufanya mazoezi yako binafsi, kisha unafanya na yale unayoelekezwa na kocha na baadae unajituma zaidi ya uwezo wako ili kuifanya timu ishinde, lakini kuna watu ambao wanakua karibu na kocha, kwa ajili ya ubinafsi wao au kwa vile wana malengo yao wanaanza kumjaza kocha maneno, na kwa vile nae ni binaadamu anaanza kufatilia mabaya unayofanya zaidi ya kutazama yale mazuri uliyofanya, hivyo matokeo yake unakua unacheza kwa presha kubwa sana na kushindwa kujua ufanye nini ili kila mtu aridhike”
    Kuna muda nilisumbuliwa sana na majeraha, ila kwa sasa hivi sina tena hilo tatizo na ninaomba Mungu anisaidie nisiumie na kupata majeraha makubwa tena, kila mara nilikua nacheza kwa tahadhari kubwa ili nisijiumize tena.
ALIPOKUA MAJERUHI
         Uhuru ambae mwanzoni mwa msimu alikua akiichezea timu ya Coastal Union kwa mkopo aliendelea “Hakuna asiejua kwamba ninaipenda sana kazi yangu, ninajitahidi sana kujituma niwapo uwanjani, na kujichunga nikiwa nje ya uwanja. Kazi yangu ni kucheza soka, na nimekua najituma sana kuongeza kiwango changu kila siku. Lakini kusema ukweli hadi sasa hivi sijui Simba wanataka mchezaji wa standard gani ili waridhike na kiwango chake, kwani mara nyingi unaona kile unachofanya ni bora zaidi ya wanachofanya hao wanaosifiwa, lakini bado wanakupa lawama na maneno ambayo yanakatisha tamaa zaidi ya kujenga! hua ninatazama sana kanda za michezo ya Simba kila baada ya kwisha, ili niangalie kama kuna makosa nirekebishe, lakini hua naona wenzangu wamefanya makosa mengi zaidi yangu,hawaambiwi kitu, ila mimi nikifanya kosa moja tu  inakua kama ni mimi ndio niliyesababisha matokeo kua tofauti”
UHURU AKIFANYA MAZOEZI BINAFSI
     “Ninashukuru sasa hivi niko huru, na Mungu kanisaidia hadi sasa majeraha yaliyokua yakinitesa muda mrefu yamepona hivyo niko vizuri na ninafanya mazoezi yangu binafsi ili nijipange na maisha mapya baada ya kumalizana na jinamizi la msimu uliopita, nipo nyumbani Mbeya ninatarajia Mungu akipenda niende kujaribu kucheza nje ya nchi, kama itashindikana nitasajili timu nyingine yoyote nifanye kile mabcho ninajiamini nina uwezo wa kukifanya kwa ubora zaidi.”

No comments:

Post a Comment