Friday, 19 September 2014

Beno kakolanya
    TZ PRISONS ONE

Baada ya katikati ya msimu uliopita kuondokewa  na aliyekua kipa nambari moja wa Tz Prisons, Wilbert Mweta, mashabiki wa soka walitegemea timu hiyo itashuka daraja, kwani katika mzunguuko wa kwanza, ilikua ipo chini kabisa mwa msimamo wa ligi, hivyo kuondoka tena kwa kipa tegemeo kuliwapa wasiwasi wengi.

  Lakini kocha David Mwamaja aliamua kumuamini kipa mwingine, Beno Kakolanya ashike hatamu za timu hiyo,  na hakumuangusha, kwani alipigana kiume na kuisaidia timu yake kuondoka katika janga la kushuka daraja. Hata katika mchezo waliocheza na Ashanti mjini Morogoro, ambao kama wangefungwa wangeshuka daraja yeye ndie alikua nyota wa mchezo, aliokoa michomo mingi na hatari nyingi.
BENO KIWA MAZOEZINI

        “Timu yetu ni nzuri, na tuko vijana wengi ambao tunaelewana, msimu uliopita haukua wetu lakini ka matayarisho tunayofanya natarajia tutakua vizuri msimu huu tofauti na uliopita” aliongea Beno “na kocha anatupa mafunzo ambayo tunamuelewa, hivyo hkuna sababu ya kutoa visingizio tena msimu huu”
  Mchezo wao wa kwanza wanacheza na Ruvu Shooting “ tumejitayarisha kwa michezo yote, tunaanza na Ruvu kisha tunacheza na Yanga, mechi zote kwetu ni ngumu lakini kwa matayarisho tunayofanya, tunaamini tutafanya vizuri katika michezo hiyo” aliongeza.

KIKOSI CHA TZ PRISONS
       Beno mzaliwa wa Sumbawanga mkoani Rukwa anasema anafurahia kuwepo kwake katika timu hiyo ya Tz Prisons “ hapa nina amani sana kwani wote tunajua malengo yetu, matarajio yangu siku moja na mimi nipate bahati nionekane na nichaguliwe katika timu ya taifa, kwani ninaamini uwezo wangu ni mkubwa sawa sawa na hao wanaocheza katika timu hiyo ya taifa” aliendelea “ nia yangu siku moja niende nje nikaceze mpira wa klipwa, hapo nitakua na manufaa kwangu mwenyewe na kwa taifa pia, na hilo najua linawezekana, bado sijafika mwisho wa safari yangu” alisisitiza.
AKIWA ACADEMY YA MBASPO

     Alisoma shule ya msingi Mwenge  Sumbawanga , na sekondari alianza Kanda huko huko sumbawanga na kumalizia katika sekondari ya Samora jijini Mbeya. “nilipokua shule nilikua nacheza soka na ndipo nikachukuliwa na Academy  ya Mbaspo na huko nikashiriki mashindano mengi, nilienda Copa Coca Cola nikiwa nimeonekana katika Academy hiyo, baadae mwaka jana mwezi wa sita  ndio nikahamia Tz Prisons ambayo nipo hadi sasa,na katika msimu huo nikacheza michezo 18 ya ligi” alisema Beno.
     Anasema ligi msimu huu ni ngumu, lakini anaamini hata timu nyingine zitakuja na tahadhari pindi wanapochza na Tz Prisons “ tupo vizuri sana na tunategemea kuongezeka uzuri ligi inavyoendelea” alimalizia Beno.

No comments:

Post a Comment