KARIBUNI
MBEYA CITY INAWASUBIRI
Ilishika nafasi ya
tatu, hakuna aliyetegemea hilo, lakini
liliwezekana, na sasa hivi inatarajia
kwenda juu zaidi. Ni kazi ngumu, ukichukulia timu zote zitakua zinaipania Mbeya
City, kwani wanajua wakifanya makosa muziki wa City ni mkubwa , wataadhirika.
Lakini nayo matayarisho yake si haba,
ingawa walifungwa na Vipers lakini sio kipimo kwamba hawako vizuri, timu
imetulia na iko vizuri zaidi ya msimu uliokwisha. Kocha mkuu wa timu hiyo Juma
Mwambusi anafurahia kikosi chake kilivyo
“ nashukuru Mungu timu iko salama na imefanya mazoezi ya kutosha, tumejitahidi kurekebisha
makosa madogo madogo ambayo yalitugharimu msimu uliopita, hivyo sasa hivi tuko
imara zaidi”
![]() |
| KOCHA MWAMBUSI |
Alipoulizwa makosa yenyewe ni kama yapi
akasema “ mfano tulicheza na Azam katika mzunguuko wa kwanza Dar, tayari tulikua
tunaongoza 3-2, na dakika zilikua zimekwisha.
Mchezaji wetu akawa kaumia, ila mpira tulikua nao sisi, wachezaji wangu hawakua
na uzoefu kwani waliendelea kushambulia kwani waliona kuna nafasi ya kupata bao
la nne, lakini matokeo yake Azam
walipookoa wakafanya shambulizi kali counter attack na kupata bao la
kusawazisha” aliongea kwa masikitiko “ wangekua na uzoefu, wangeutoa mpira nje
ili mwenzao atibiwe na kisha mchezo ungepoa na dakika zingemalizika kwa
ushindi, lakini ndio hivyo, sasa hivi wana uzoefu wa kutosha makosa kama hayo
sidhani kama yatatokea tena”
“ Kitu ninachofurahia, hakuna mchezaji
aliyeondoka, wote wapo na pia tumeongeza nguvu kwa kumleta Themi Felix toka
Kagera akasaidiane na kina Mwegane kule
mbele, tunajua uzoefu wake katika ligi utatusaidia kupata matokeo mazuri, maana
ni mfungaji mzuri sana, naweza sema ni mmoja kati ya wafungaji bora Tanzania. Pia
tumemuongeza kiungo Peter Mwalyanzi kutoka Mgambo JKT.
Alipoulizwa kama anafikiria kupata ubingwa
sasa hivi akasema “ hapana, siwezi kuahidi kitu kama hicho, msimu uliopita
hatukuahidi kitu na tazama tulipofikia, na sasa hivi hatuahidi kitu, ila tuna
uhakika tutafanya vizuri sana, Hua
napenda kuichukulia kila timu ninayokutana nayo kwa uzito mkubwa, hivyo kwangu
mimi kila mchezo ni fainali, napenda niwe najipanga kwa mchezo unaofuata, najua
tutafika kila mmoja anapotamani kufika”


No comments:
Post a Comment