Timu ya Tz Prisons,
ilizima kelele za msemaji wa timu ya Ruvu Shooting Masau Bwire, baada ya kuwafunga kwa
mabao mawili kwa bila katika mchezo mzuri uliochezwa uwanja wa Mabatini Ruvu.
Tz Prisons ambayo
katika mchezo wake wa mwisho wa majaribio kabla ya kuanza kwa ligi, walipoteza
kwa idadi kama hiyo ya magoli dhidi ya JKU ya Zanzibar, waliutawala mcheezo kwa
kipindi kirefu, na magoli yao yalifungwa na
Laurian Mpalile na Jacob Mwakalobo. Tz Prisons mchezo unaofuata
watacheza na timu ya Yanga jijini Dar.
xxxxxxxx
Ndanda FC ya Mtwara, imeanza vizuri ligi kuu ya VODACOM baada ya kuwafunga wageni
wenzao katika ligi hiyo Standa United kwa jumla ya mabao 4-1 katika mchezo
uliochezwa katika uwanja wa Kambarage Shinyanga..
Ndanda ilipata mabao yake la kwanza likifungwa
na Paul Ngalama katika dakika ya 16 ya mchezo. Bao hilo liliwafanya Stand
kucheza kwa kutokujiamini na kupoteza mipira mingi bila sababu.
Katika dakika ya 35 Nassor Kapama aliipatia
timu ya Ndanda bao la pili kutokana na mabeki wa Stand kushindwa kuzuia
mashambulizi ya Ndanda, lakini dakika
moja baadae Stand wakapata bao lililofungwa na Salum Kamana.
Dakika tano baadae wakafungwa goli la tatu
lililofungwa na Ernest Josef. Kwa ujumla kipindi chote cha kwanza Ndanda
waliutawala mchezo huo na kuweza kupata mabao hayo matatu.
Kipindi cha pili Stand walionekana
wamepata uhai na kuweza kuzuia mashambulizi ya Ndanda, lakini dakika ya 90
Ndanda walipata bao la nne na kuufanya mchezo huo kumaliza kwa ushindi wa mabao
4-1.
xxxxxxxxxx
Timu ya Yanga, imeanza
vibaya ligi ya Vodacom Tanzania baada ya kufngwa magoli mawli na timu ya Mtibwa
ya Morogoro. Katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Jamhuri Morogoro,
unawezakusema sababu kubwa iliyofanya Yanga kupoteza mchezo huo ni ubovu wa
uwanja huo.
Mtibwa walipata bao la kuongoza katika dakika
ya 16 lililofungwa na Mussa Hassan Mgosi
baada ya kuwahi mpira mrefu uliopigwa na Ame Said na kuubetua ukampita
kipa wa Yanga Deo Munishi.
Yanga walijitahidi kupata bao la
kusawazisha lakini ikawa ngumu, kwani hakukua
na ufundi kutokana na ubovu wa uwanja hivyo kuwashinda wachezaji wa Yanga
waliozoea kucheza pasi fupi nyuma na
kisha kupiga ndefu kuwapelekea wachezaji wao wa pembeni. Mpira muda mwingi
ulikua ukibutuliwa tu na hauna ladha.
Kipindi cha pili Yanga walikianza kwa kasi
na kufanikiwa kupata penati dakika za
mwanzo tu lakini mshambuliaji wake hatari Toka Brazil Jaja alishindwa kufunga
baada ya kipa wa Mtibwa kkuokoa kwa
mguu.
Katika dakika za mwisho za mchezo huo Ame
Said aliyecheza vizuri katika mchezo huo aliipatia Mtibwa bao la pili baada ya
kkupokea pasi ndefu na kumuhadaa beki wa Yanga Nadir kisha akapiga kiufundi
mpira uliomshinda kipa wa Yanga. Hadi mwisho Mtibwa 2 na Yanga hawakupata kitu.
Mabingwa watetezi Azam Fc imeanza vizuri lig hiyo baada ya kupata ushindi mzuri wa mabao matatu dhidi ya moja la Polisi Moro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Azam Chamazi.
Mabingwa watetezi Azam Fc imeanza vizuri lig hiyo baada ya kupata ushindi mzuri wa mabao matatu dhidi ya moja la Polisi Moro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Azam Chamazi.
Magoli ya timu hiyo mawili
yalifungwa na mshambuliaji mpya wa timu hiyo Didier Kavumbagu aliyefunga moja
kila kipindi na moja likafumgwa na Agrey Morris.
xxxxxxxx
MATOKEO
KAMILI YA MZUNGUUKO WA KWANZA NI
MBEYA
CITY 0 JKT RUVU 0
STAND
UNITED 1 NDANDA FC 4
RUVU
SHOOTING 0 TZ PRISONS 2
MGAMBO 2 KAGERA 1
AZAM FC
3 POLISI MORO 1
SIMBA 2
COASTAL UNION 2
MTIBWA 2
YANGA 0



No comments:
Post a Comment