Friday, 26 September 2014

SIMBA NA YANGA YAAHIRISHWA

SIMBA NA YANGA SASA OCTOBA  18

Shirikisho la soka Tanzania, TFF limesogeza mbele kwa wiki moja mchezo wa mahasimu wa jadi Tanzania, Yanga na Simba kwa wiki moja zaidi, na hivyo sasa utafanyika tarehe 18 octoba badala ya tarrehe 12 kama ilivyokua katika ratiba ya awali.. 

Akielezea sababu zilizofanya  kusogezwa mbele kwa mchezo huo, mkurugenzi wa mashindano wa TFF Boniface Wambura amesema imetokana na kuingiliana na ratiba ya FIFA ambapo kwa tarehe hiyo timu ya taifa ya Tanzania itacheza na timu ya Benin.
    Kumekua na maoni tofauti kutoka kwa mashabiki wa timu hizo, wa Yanga wakisema hiyo imetokana na TFF kutaka kuwasaidia Simba ambao kwa muda mfupi wamepata bahati mbaya ya wachezaji wake watano muhimu kuumia, hivyo waliogopa iwapo watacheza bila ya hao wachezaji kuna uwezekano mkubwa kwa tiu hiyo kupoteza mchezo.
    Kauli hizo zimepingwa vkali na mashabii wa Simba, wakiongozwa na mwenyekiti wa usajili wa timu hiyo Zacharia Hanspope ammbae alisema timu yake iko vizuri idara zote, na kama kuumia kwa hao wachezaji, wapo wengine wenye kiwango kama hicho ambao wanaaminiwa watafanya vizuri kama wakipata nafasi, aliongeza kwamba timu yake haiwaogopi Yanga hata wakiamshwa usiku wa manane wapo tayari kucheza nao na wana uhakika watashinda.

No comments:

Post a Comment