Wednesday, 1 October 2014

MATOGORO, MCHEZAJI BORA WA MWEZI SEPTEMBER

matogoro,mchezaji bora wa mwezi September

Bodi ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania, imemchagua Anton Matogoro waMbeya  City kuwa ni mchezaji bora wa ligi hiyo kwa mwezi September 2014. Amepata na zawadi ya pesa kiasi cha shilingi milioni moja.

    Anton,  kiungo wa chini wa timu hiyo, amefanikiwa kuchaguliwa baada ya kucheza katika michezo miwili ya ligi hiyo, wa kwanza ilikua na JKT Stars na wa pili ukiwa wa Coastal Union.

   Anton ana uwezo mkubwa wa kupiga pasi, ziwe fupi ndefu na pia anajua sana kuziba nafasi ili kupunguza mashambulizi, alistahili kuchaguliwa hata katika ligi kuu iliyokwisha, kwani katika mchezo waliocheza na Azam jijini Dar, alitawala sana sehemu ya kati kati na kuwapa wakati mgumu viungo wa Azam.   Na hata katika mchezo waliocheza na Yanga jijini Dar,pamoja na kua pungufu baada ya kuolewa kiungo mwingine Steven Mazanda, bado alimudu kutawala sehemu  ya katikati na kufanya awe nyota katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment