Monday, 24 February 2014

PETER MICHAEL
wa tz prisons

    Katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, timu ya Tz Prisons haikua inaenda vizuri, ilikua inasua sua mno, baadae wakaamua kubadili benchi la ufundi kwa kumuondoa kocha Jumanne Chale na kumleta kocha mzoefu David Mwamaja. Hali hiyo kwa kiasi Fulani imeleta mabadiliko kwani katika michezo mitano ya mzunguuko wa pili, imetoka sare miwili na kushinda mitatu.

      Juhudi kubwa zinafanywa na wachezaji na benchi la ufundi kuhakikisha hawapotezi hata mchezo mmoja katika mzunguuko huu wa lala salama.
      Mmoja kati ya wachezaji wa timu hiyo ambae ana kiu ya kuhakikisha hilo linafanikiwa ni Peter Michael, mshambuliaji anayejua goli liko wapi, kwani katika msimu huu wa ligi hadi sasa ana magoli nane na bado ana hamu ya kuongeza mengine.
PETER MICHAEL AKIZONGWA NA NYOSO

      “Ninajitahidi sana kushirikiana na wenzangu ili tuweze kufanikisha hilo, kwani hata mashabiki wetu walikua wametukatia tamaa kutokana na matokeo mabovu, siwalaumu hao mashabiki, hakuna mtu anaependa timu inayofanya vibaya, na sisi ili kuwaita tena ni kujitahidi kucheza vizuri na kupata ushindi, hapo nina uhakika mashabiki wetu watarudi na kutupa sapoti ya nguvu” alisema Peter Michael.
PETER NA NYOSO

       “Tazama michezo yetu ya mzunguuko wa pili, tumetoka sare na Coastal Union, tukawafunga Ruvu, kisha tukawafunga Mtibwa kwao, baadae tukawafunga JKT na mwisho tumetoka sare ya ajabu na Azam ambayo kama mwamuzi angechezesha kwa haki nina uhakika tungeshinda” aliongeza Peter.
        Peter Michael alizaliwa Dar na kusoma shule ya msingi Juhudi na sekondari akasoma katika shule ya Makongo. Alikua akicheza soka shuleni Makongo, na uswahilini akiichezea timu ya Mti Pesa Fc ya Ukonga.
PETER  MICHAEL(mwenye tshirt)AKIWA NA JIMY SHOJI.
         Mwaka 2011 akajiunga na Tz Prisons, na katika msimu huu hadi sasa tayari ana magoli nane mfukoni,   kishawafunga Yanga goli moja, mtibwa kawafunga mara mbili,kisha akawafunga Mgambo, aliwafunga Azam jijini Mbeya,Ruvu shooting na mawili akawafuga  Ruvu Stars katika ushindi wa magoli sita bila.
       “Kinachonisaidia kufunga ni kutokana na kucheza na ‘mafundi’ kama Jimmy Shoji ‘Gema’,  Salum Kimenya,na Omega Seme pamoja na wachezaji wengine tuliopo pamoja, maana tumezoeana sana hivyo  inakua rahisi hata kutengeneza hizo nafasi”.
AKIWA NA WACHEZAJI WENZIE

           Akaongeza  “sasa hivi timu yetu imeshika kasi, ingawa hata mzunguuko wa kwnza tulikua tkicheza vizuri, lakini sasa hivi tunapata na matokeo, hivyo tutajitahidi sana kuendelea ushinda ili tujiweke katika nafasi nzuri” kisha akaongeza “Tunawaahidi mashabiki wetu mambo mazuri yanazidi kuongezeka, kila ataekuja mbele yetu tunapigana nae tumshinde, waje kuona timu yao inavyocheza mpira unaopita katika njia, kwa sasa hivi Tz Prison tuko vizuri sana” alimalizia Peter Michael.

     

2 comments: