Sunday, 2 March 2014

Simba yazinduka

Simba imezinduka baada ya kuifunga  Ruvu Shooting kwa magoli  3-2, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Hadi mapumiko Simba walikua wakiongoza kwa magoli mawili yote yakifungwa na Amis Tambwe.

     Alifunga la kwanza katika dakika ya 25 baada ya kuuwahi mpira wa adhabu uliopigwa na kiungo chipukizi wa Simba Said Hamis Ndemla na kipa wa Ruvu alishindwa kuudaka, na alipoutema ndipo Tambwe akauwahi na kufunga.
         Na la pili alifunga katika dakika ya 35 kwa kuunganisha krosi nzuri iliyopigwa na beki wa kulia wa Simba, anaejituma na kupanda mbele kila mara,  Haruna Shamte .
         Ruvu Shooting walicheza vizuri katikati lakini walikuwa wakishindwa kulifikia lango la Simba  kutokana na ushirikiano mzuri uliokua ukifanywa na walinzi wa Simba wakiongozwa na Josef Owino na Don Mosoti.
          Hadi mapumziko matokeo yalikua ni Simba mawili na Ruvu hawakupata kitu.
    Kipindi cha pili Ruvu walikianza kwa kasi na walikua wakionyesha dhahiri wanataka magoli, na walifanikiwa kupata goli la kwanza kupita kwa Said Dilunga katika dakika ya 75 akiunganisha kona iliyochongwa na  Michael Pius.
    Kabla hawajashangilia vizuri kiungo mshambuliaji wa Simba Harun Chanongo alifunga bao la tatu katika dakika ya 78, baada ya kupokea pasi toka kwa mkongwe Amri Kiemba.
       Ruvu hawakukata tamaa na katika dakika ya 82 Jerome Lambele aliyeingia badala ya Elias Maguri aliifungia timu yake bao la pili kwa njia ya penati baada ya mchezaji mmoja wa Simba kuushika mpira katika eneo la hatari.

1 comment: