Thursday, 6 March 2014

yanga na ahly kucheza Alexandria

    Mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Al Ahly ya Misri umepangwa kufanyika katika uwanja wa  Harras el Hadoud uliopo Alexandria Misri  siku ya jumapili, badala ya jijini Cairo.
        Waziri wa mambo ya ndani wa Misri alipiga marufuku mchezo huo kufanyika jijini Cairo baada ya mashabiki wa Al Ahly kufanya fujo na kujeruhi polisi 26 mara baada ya kwisha kwa mchezo kati ya Al Ahly na Saxien ya Tunisia. Mchezo huo umepangwa kufanyika bila ya mashabiki.
        Mkurugenzi wa Al Ahly, Sayed El Hafez alipanga kuongea na uongozi wa Yanga kuhusiana  na mabadiliko hayo ya uwanja kwani kulikua na tetesi kwamba Yanga wasingekubali kucheza nje ya Cairo.
 Al Ahly walipoteza katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Dar kwa goli moja kwa bila

1 comment:

  1. Mechi hii Yanga wananafasi kubwa ya kusonga mbele, wanachotakiwa ni kuwa makini tu. Uwezo wanao wanatakiwa kuweka nia pamoja na kuwa makini mchezoni

    ReplyDelete